22.11.13

Saturday, August 04, 2012

ROMA APATA AJALI MBAYA NA GARI LAKE AKIELEA MOROGORO KWENYE SHOW

Muda mchache uliopita msanii wa kizazi kipya kwenye bongo hip hop ROMA amepata ajali mbaya barabara ya Morogoro. Roma anasema alikuwa yupo kwenye mwendo wakawaida ndio tairi la mbele lilipopata pancha na ndipo gari likaacha njia yake na kwenda kugongana uso kwa uso na fuso ambalo lilikuwa upande wa pili na gari hilo dogo alilokuwa akiendesha Roma kurudi lilipotokea.
Roma ananiambia kwa sasa anaelekea Hospital kwa check up zaidi ila aliokuwa nao kwenye gari hakuna aliyeumia wote ni wazima.

Roma akimwelezea police wa usalama barabarani kilichotokea mpaka kupata ajali hiyo mbaya.

 Huyu ni mmoja kati ya marafiki wa Roma aliyekuwa nae kwenye gari wakielekea Morogoro kwenye show

7 comments:

Anonymous said...

POLE SANA ROMA TUSHUKURU MUNGU HAKUNA ALIEUMIA. MDAU DODOMA

Anonymous said...

oh pole sana jembe letu roma

Anonymous said...

daa thenx God coz jembe yupo fine.. polee sana mzazi....

Anonymous said...

Pole xana' djembe

Anonymous said...

pole sana jembe tumshukulu Mungu mpo wazma wote

Anonymous said...

Pole sana roma

Unknown said...

dar..hii noma !!!!