22.11.13

Tuesday, January 08, 2013

INAWEZEKANA KAMA MIMI NA WEWE TUTAAMUA!! "ROMA"

Jana nimeweka chart ya dj choka ya HULKSHARE inayoonyesha kuanzia tarehe 4 january hii siku ambayo ameiweka net track ya ROMA ya 2030 hadi jana usiku nyimbo hiyo ilikuwa imeshasikilizwa online na watu 18140, na ikiwa watu takribani 9215 wame udownload!! 

Sasa imagine kama ingekuwa kila aliye download ngoma hii anailipia tsh 3000/= kama awali nilivyofanya japo sio kwa njia hii, basi 2030 ingekuwa imeshaingiza ths 27645000/= milioni ishirini na saba na laki sita na elfu arobaini na tano kitu kama hicho!! au ingekuwa kila anayedown load anatoa 1000/= basi ingekuwa ni tsh 9215000/= yani milioni tisa!! hapo bado hatujahesabu wale waliosikiliza tu, nao tufanye labda wanachangia jero jero sasa zidisha 18140 mara 500/= inakuja kama milioni tisa hivi naaa...hahahahahha KWANI PIA TSH 500 INATUSHINDA? KWA NYIMBO 1?
Na hiyo ni kwa site hii moja tu!!! so ndani ya siku 3 tu ningekuwa nimeingiza tsh milioni 27/= au hata hiyo milioni tisa!!!na zaidi...
SASA UMEONA KAMA YANAWEZEKANA EEE? KAMA TUKIAMUA LAKINI MIMI NA WEWE!!!...basi kuna uwezekano huu mziki unalipa sana kuliko hata wafanyakazi wengi wa mashirika ya uma, japo inaweza ikawa malipo ya muda mfupi!!
TUFANYAJE SASA MARAFIKI KWA TAKWIMU KAMA HIZI? ikiwa tunadownload bure na show tunaingia free!!!!

5 comments:

Anonymous said...

Roma hio pesa nikubwa sanaa usifanye mzaha 3000? bora uombe tu km unataka msaada,ebu jiambie mwenyeo kwanza ule wimbo ni wa kukuingizia milioni 27 kwa siku 3? jibu hapana.na je ni wimbo wa kukufanya usiingize milion 15 mpaka utakapotoa nyimbo nyengine? jibu hapana,sasa bac km munataka hili punguzeni iyo hela baada ya 3000 iwe 250(mia mbili hamsini)tena iwe wasanii wote coz ukifanya ww tu utakuja jikuta nyimbo yko watu hawaijui coz hawanunui si nyimbo nyengine ni bure.

Anonymous said...

kama wa mitandao ya cm wanauza 300 ambao unaendelea kubaki kwao, bac na nyie wasanii fanyani jero kwa kuanzia tuone lkn buku 3 cyo wote wanaoweza kuaford ni wazo tu,

Unknown said...

dah...kwa upeo wngu. me naamin inawezeka.
sema kinachotakiwa wadao wote wa mziki wetu tuwe teal kujitia kwa namna yoyote ili...ili tuweze kufikisha mziki wetu na wasaa wetu ktk stage nyingine.
*#mziki ni kazi tena kazi ya akili na uwezo binafs..
ni kwa muono wngu tu.

wamitulinga said...

ROMAAA HII KITU NI NZURI NA INALIPA SANA, LAKINI INATAKA KUJIPANGA SANA TENA KWA WASANII WOTE WALAU 300TSH KWA KILA WIMBO NA ZIWEPO OPTION ZA KUUDOWNLOAD,KUTUMIWA KWENYE WHATSAPP, NA PIA HATA KUUPELEKA KAMA PUSH KWENYE MITANDAO YA SIMU ILI KILA MTZ MWENYE AINA YEYOTE YA SIMU AWE NAO. NI HAYO TU........MOSES SAMWEL RYOBA..HEAVY EQUIPMENTS OPERATOR,DOZER,EXCAVATOR,LOADER-UKONGA BANANA,DAR. 0757430913

Mwakitenge said...

Inawzekana cha kufanya tutengeneze music database kubwa na kutafuta sponcer tena hawa wa mitandao ya simu then tunatengeneza web application kama hulkshare juu yake lakin yenyewe inakuwa ni online music store ila bei ya nyimbo isizidi buku