22.11.13

Friday, February 22, 2013

WEZI WAITEMBELEA STUDIO YA PROD MBEZI NAKUSOMBA KILA KITU MUHIMU.

Mida ya saa kumi nilitoka kwenda tizi kwa maana hua nachezaga basketball, nikafunga studio vizuri nikaenda kwenye kikapu kurudi mida ya saa moja kasoro saa kumi na mbili hivi nimefika tu mlangoni nikakuta mlango upo wazi kabisa nikajua hapatayari wamefanya yao wezi nikaingia ndanikukagua kama wamesafisha studio nzima au wamenisamehe vingine ndo nikagundua wezi wameiba vitu vya kubebeka fasta fasta kama Laptop aina ya gateway touch screen, head4n za studio,speaker pamoja na external ilikua pia pale juu.Vitu vyote hivo vinagarim zaidi ya milion 1,na extenal waliobeba ilikua na kazi za wasanii za kutoka this february lkn leo asubuhio nimepata backup ingine japo sio data nyingi.

Kazi zilizoenda na maji ni kama kazi ya Chiddi Benz, Peter Msechu, Noorah na nyingine nyingi tu, nimeshatoa taarifa polisi na wanashughulikia hilo simuhisi mtu yeyote yule kwa sababu sina ugomvi na mtu yeyote yule

No comments: