22.11.13

Wednesday, May 29, 2013

(News) NIMETUMWA NA KAMATI YA WASANII NISEME HIVI:

Katika kikao kilichokaa leo jioni pale LIDARZ CLUB cha wasanii na ndugu wa marehemu ALBERT MANGWEA mimi kama DJ CHOKA nimeteuliwa niwe natoa habari zote za msiba kwenye SOCIAL NETWORK. Sasa basi kila kitu kitakachoendelea kuhusu msiba wa ndugu yetu MANGWEA mimi nitakuwa nawajulisha LIVE.

Kamati imenituma niwaambie ndugu zangu watanzani kuhusiana na hizi habari zinazoendelea kwenye SOCIAL NETWORK kuanzia blog mbali mbali kuwa marehemu amefariki kwa kula unga mwingi au kujidunga madawa ya kulevya, familia na kamati inawaomba msidanganyike na habari hizo wanaomba muwe na subira kidogo hadi barua rasmi itoke hospital na ndio watasema kuwa marehemu alifariki kwa kitu gani.

PICHANI NI WASANII PAMOJA NA NDUGU WALIOTEULIWA KUWA KWENYE KAMATI YA MAZISHI. 

2 comments:

Anonymous said...

Poleni sana jamani

Anonymous said...

da .Lord give us,then took him away.R.I.P.Albert.