22.11.13

Wednesday, June 12, 2013

(Audio) PEWA ABAGENGE AWADISS NONINI, HUDDAH MONROE, OCTOPPIZZO NA SIDIKA


Msanii kutoka Kenya aitwaye Pewa Abagenge,inaonekana hajamaliza beef yake Na Godfather wa Genge(NONINI),katika wimbo wake mpya ambao ameutoa wiki hii anasikika akikashifu ma presenter ambao pia ni wasanii.Nchini Kenya wasanii wengi chipukizi wamekuwa wakilalamika kwamba  presenter ambao pia ni wasanii hawachezi ngoma zao kwa kuogopa competition,Hii inajidhihirisha sana kati ya Pewa Na Nonini,kwani wanafanya mziki aina moja na la kustajabisha ni kwamba mziki wa Pewa hauchezwi kamwe kati show ya Nonini na pia FM ambako Nonini anafanya kazi yake.Nikinukuu kutoka kwa wimbo wenyewe amesema

Hii sanaa ina Ufisadi inashinda hata serikali,
Promo ngoma mbaya ,wanakanyagia kali,
Presenter ni msanii anaogopa competition
Kwa jina la Baba mi  nakemea roho chafu
Katika wimbo huu pia amemtaja Huddah Monroe,binti aliyekuwa kwenye BBA ya mwaka huu wa 2013 na kuondolewa baada ya wiki moja,amekashifu tabia potovu ambazo mabinti wa Kenya akiwemo Huddah, Sidika na wengineo Wameingilia huku wakijiita  socialite ilhali ni utovu wa nidhamu,huku akimsifu Kethi, binti wa aliyekuwa Seneta Wa Makueni Nchini Kenya kwa ushujaa aliouonyesha wakati wa Kesi ya Urais nchini Kenya.Wale waliouza nafsi zao ili wawe mabingwa kwa industry pia hawajaponea kukemewa na msanii huyu,hapa inaonekana anamwashiria gwiji wa hiphop Octoppizzo na wasanii wengine wanaojulikana nchini Kenya walioko katika dini la Free Mason.
  Jambo lingine pia hajakosa kunena kuhusu mabinti wakenya waliopatikana wakishiriki porn na mbwa mjini Mombasa,Pia maovu yanayotendeka serikalini,anasikika akisema “
Wengi wameuliwa Kesi Zao mahakamani,
Tume za uchunguzi ni miradi ya serikali,
Kesi imelipiwa mwenye kesi haonekani,
Kwa jina la baba mi nakemea Ufisadi”
Wimbo huu kwa hakika utawagusa wakubwa walioko kwenye serikali pia  wadogo mitaani,
SIKIZA WIMBO WENYEWE UTOE UAMUZI WAKO MWENYEWE. Katika wimbo huu amemshirikisha Jokay,msanii chipukizi toka tanzania
 Nakemea –Mistari
  Pewaaaa Abagengeeeee
   Jokay…. Eeeeeeh
   Kusini Recordz………………
Hii sanaa ina Ufisadi inashinda hata serikali,
Promo ngoma mbaya ,wanakanyagia kali,
Presenter ni msanii anaogopa competition
Kwa jina la Baba mi  nakemea roho chafu
Its only in Nairobi Kahaba anajiita socialite,
No Love for Huddah,Sidika ameonyesha uchi,
Mwanamke ni akilia makofi napigia Kethi,
Kwa Jina LA Baba mi nakemea ukahaba,
Wasanii wanauza nafsi ngoma zao ziingie chati
Swaga Ni Bandia wanajiita Illuminati,
Sikiza ngoma zao wanasifia shetani,
Kwa jina la baba Nakemea Free Mason.
Miujiza Kanisani mi ndio Pastor Njoroge,
Imani ni Lazima geuza mdomo kama mwende,
Gospel biashara shetani anapigwa Teke,
Kwa jina La Baba mi nakemea ma hypocrites.

Yote nayoyaona unfair leo nayakemea,
Inanibidi kusema ila wengine watanielewa vibaya*2

Wakenya ni Wazembe wanalaumu serikali
waiting for Kenyatta awabaie makali,
Stress inawamaliza wana Rwanda kaa Kigali,
Kwa jina la baba mi nakemea mauzembe,
Mombasa ni sodoma gomorah mi inanitisha
Alikuwa mlinzi siku hizi anafanya mapenzi,
Naongelea mbwa dada zangu mnakosea,
Kwa jina la baba mi nakemea immorality
Mapenzi ni kaa maua bt siku hizi yananyauka,
Wachache wanapenda wengi roho zinavunjika,
Mwanamke ni wako kwa rafiki yako anamegeka
Kwa jina la baba mi nakemea ma player,
Giza Nairobi Kenya Power kuna Nuru,
Biashara niya mshumaa wakenya wanalipa ushuru,
Faida mnapata but wenzetu inatudhuru,
Kwa jina la baba mi nakemea monopoly

Yote nayoyaona unfair leo nayakemea,
Inanibidi kusema ila wengine watanielewa vibaya*2

Wengi wameuliwa Kesi Zao mahakamani,
Tume za uchunguzi ni miradi ya serikali,
Kesi imelipiwa mwenye kesi haonekani,
Kwa jina la baba mi nakemea Ufisadi
Mtoto wa miaka kumi mja mzito  miezi tisa
Nani mtamlaumu saa wazazi washalegeza
Ngono mtaani siku hizi mchezo wa kuigiza
Kwa jina la baba mi nakemea mafisi
Wengi wamesoma wamepata degree
Ndugu yako ndio kazi karatasi haisaidii
Wanjala kimani musyoka na otii
Kwa jina la baba mi nakemea ukabila
Siasa ni siasa wanasiasa ni siasa
Nguruwe atakula bt hakuna siku atasaza
Kweli ni ukweli basi fight on ALAI
Kwa jina la baba mi nakemea tama

Yote nayoyaona unfair leo nayakemea,
Inanibidi kusema ila wengine watanielewa vibaya*4

No comments: