YOUTUBE LINK : http://youtu.be/cNKfC1P9i00
DOWNLOAD LINK:http://www.hulkshare.com/st5q1eqtq4g0
Bosco Baya ni mzaliwa
wa pwani ya Kenya na msanii wa mziki wa kizazi kipya.Anafahamika kwa
miondoko ya kivyake ,uimbaji wake na staili anayotumia kwa uwasilishaji ujumbe
ni wenye hisia na unaogusa.Alisomea shule ya upili ya Mt.Terezia, iliyo kaunti
ya kilifi alikozaliwa.
Amelelewa na Mama
yake kwa shida na raha….anadai kumpenda sana mama yake kuliko chochote kile.Kijana
huyu mcheshi mwenye miaka ishirini na nne yuko katika mikataba na kituo cha
kurekodi cha Kusini Rekodi Kilicho kati kati mwa jiji la Nairobi.
Alianza mziki rasmi
miaka ya 2005 ,akiwa kidato cha pili.Alizinduliwa na Tino The Don producer
anayezindua na kukuza vipaji nnchini Kenya kaunti ya kilifi.Aliingia studioni
2006 na kupata kurekodiwa na Producer aliyemahiri na aliyeboboea kwa mitindo ya
hiphop,ragga,reggae na rnb.Producer huyu
Edward Ananda anayejulikana kama Ananda1 ndiye aliyembadilisha Bosco baya
kutoka kwa mitindo ya hiphop hadi akawa mwimbaji mahiri sana wa mitindo ya
Afrofussion.
Ametambulika na
kibao chake Barua aina ya rhumba kilicho chezwa na kurekodiwa Kusini Records na
maproducer Black Child and Ananda.Kibao hicho kilicho vuma Kenya nzima kimempa
sifa zote bwana huyo.Anavibao vinavyotikisa kama Urafiki wa M-Pesa ,Siku njema
na vingi vyengine.Nimkaazi wa jiji la Nairobi na mpishi wa mikate na keki.
No comments:
Post a Comment