22.11.13

Sunday, August 18, 2013

(News) HUDUMA YA MAWASILIANO YA VODACOM YAREJESHWA

 Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Rene Meza, akizungumza na waandishi wa habari, (hawapo pichani) kuhusiana na kurejeshwa kwa huduma zote za mtandao wa Vodacom baada ya kukosekana kwa saa 16 kufuatia moto kuzuka katika kitovu cha kuendeshea mitambo jijini Dar es Salaam,Mkutano huo ulifanyika katika hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Rene Meza, akizungumza na waandishi wa habari, (hawapo pichani) kuhusiana na kurejeshwa kwa huduma za mtandao wa Vodacom baada ya kukosekana kwa saa 16 kufuatia moto kuzuka katika kitovu cha kuendeshea mitambo jijini Dar es Salaam. Mkutano huo ulifanyika katika hoteli ya Serena,Pamoja nae ni Mkuu wa kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania,Kelvin Twissa.

Taarifa kwa vyombo vya habari
Huduma ya Mawasiliano ya Vodacom yarejeshwa.
·      Ni Baada ya moto kuungunza mitambo
·      Mtandao ulizimwa kwa saa 16 nchi nzima
Dar es Salaam, Agosti 18, 2013 ……. Baada ya kukosekana kwa huduma za mtandao wa Vodacom kwa takribani masaa 16, huduma hizo zimerejeshwa katika hali yake ya kawaida asubuhi  ya Jumamosi ya Agosti 17.
Akizungumzia tatizo lililosababisha kukosekana kwa huduma za mawasiliano kwa watumiaji wa mtandao huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Rene Meza amesema chanzo cha kukatika kwa mawasiliano nchi nzima siku ya Ijumaa ni moto uliotokea katika mtambo mkuu wa kuendeshea mtandao (Main Switch) uliyoko Dar es Salaam.
 “Kufuatia hatua hiyo, hatukuwa tena na uwezo wa kutoa huduma kwa watu wote kuanzia siku ya Ijumaa jioni hadi Jumamosi asubuhi, hali hii iliathiri wateja wetu wote kwa ujumla kwani walishindwa kuwasiliana na ndugu jamaa na marafiki ambao wote ni wateja wetu, alisema Meza.

Aidha aliomba radhi kwa jamii ya Watanzania na wateja wa Mtandao wa Vodacom kwa kukosa mawasiliano katika kipindi hicho, na kusema kuwa wateja wote wa mtandao wa Vodacom watarudishiwa gharama zote kwa huduma yoyote walionunua na kuhitaji kuitumia wakati ambapo mtandao  haukuwa unapatikana, “Fidia hizi kwa wateja wetu wote zitatolewa siku ya jumatatu ya Agosti 19, 2013 alisema Meza.
 “Tunaishi katika dunia ambayo mawasiliano ni muhimu katika maisha yetu ya kila siku hivyo tunaelewa kuwa tatizo hili limekuwa kikwazo kikubwa kwa wateja wetu, Na tunawashukuru kwa kuwa waelewa na wavumilivu katika kipindi chote ambacho tumekuwa tukikabiliana na tatizo hili, alisema Meza.
Meza alihitimisha kwa kuhakakikishia Watanzania na wateja wa Vodacom kwa ujumla kuwa Vodacom imedhamiria kuendelea kutoa huduma zenye viwango vya hali ya juu nchini.
 “Ninapenda kuwashukuru wafanyakazi wetu wote na washirika wetu ambao kwa pamoja wamefanya kazi bila kuchoka katika kuhakikisha huduma zote zinarejea hadi katika hali ya kawaida hadi kufikia Jumamosi asubuhi, Jitihada zao na kazi kubwa waliyoifanya imewezesha huduma zote kurejea katika hali ya kawaida, alihitimisha Meza.
Mwisho……… 

No comments: