22.11.13

Friday, August 02, 2013

(News) KALA JEREMIAH na G-NAKO wammwagia sifa Producer JOHN B wa GRANDMASTER RECS Arusha

 PRODUCER JOHN B  
Wasanii Wenye heshima kubwa Tanzania Kala Jeremiah Mmmiliki wa tuzo Tatu za kili Music Awards Mwaka Huu na Mkali wa chorus za HipHop Toka Crew ya Weusi Hapa namsanua GNako wamefunguka exclussive kwenye short Interview waliopiga na DJ Haazu wa Mambo Jambo Radio Arusha na kumsifu Producer John B wakisema kuwa jamaa ni kichwa na haswa kwa sasa Imani yao kwa Mkali huyo wa Beat na Mchanganyaji wa Sauti Imeongezeka mara dufu baada ya Jamaa kuwakutanisha kwenye mdundo mmoja Vichwa 9 vya maana.

 KALA JEREMIAH
GNAKO 
 Ni siku chache tu toka Producer huyo aachie Prioject yake ya Life Goes On ambayo humo kati viko vichwa tisa vikali vywa muziki wa Tanzania ambao ni Kala Jeremiah, GNako, Chaba, Mo Plus, Chibo,  Ibra Da Hustler, TDX, Ordinaly na Jordan ambapo humo ndani kila mmoja kaua kivyake.
Ni ngoma ambayo kwa siku chache tu hizi toka itoke imekuwa Gumzo kwa Mtaa haswa kwa wale Wanaoufeel muziki wa Hiphop Hapa Nchini kutokana na Mistari Mikali, beat na Flow tamu zilizofanyika kwenye track hiyo.

Vichwa vyote hivyo vilikutanishwa kwenye ngoma hiyo na Producer huyo ambaye ametaja kuwa ni muendelezo wa yeye kufanya kazi na Wasanii wengi Hapa Nchini na Nje ya nmchi kwa kuwachanganya kwenye Track moja kwa ajili ya Wapenzi wa Mikono yake pamoja na Fans wa Wasanii husika kwenye track.

DJ HAAZU alitamani kusikia moja kwa moja Toka kwa Kala Kuwa kila mmoja anaizungumziaje Track hiyo ambapo wote kwa pamoja hawakutofautiana sana maelezo yao Wakidai kuwa kwanza kila Mmmoja aliumiza kichwa kuandika mistari mikali na Flow tamu kwa kuwa anajua kuwa ni vichwa vikali anavyokutana navyo kwenye ngoma moja.
FANYA KUMSIKILIZA KALA AKIFUNGUKA KUHUSU HIYO NGOMA KWA KU CLICK HAPA
AMUA KUMSIKILIZA G NAKO NAYE KWA KUCLICK HAPA

Swali lingine Kwa upande wa Wao Wanamzungumziaje JOHN B hapo ndo palikuwa patamu kwa Sababu walitiririka kwa kummwagia sifa John B wakisema jamaa ni kichwa sana na wao wamependa Idea ya jamaa kuwakutanisha kwenye ngoma moja mastar na wanatamani next time pia jamaa awatafute watakuwa tayari.

KUMSIKILIZA KALA AKIMZUNGUMZIA JOHN B CLICK HAPA

KUMSIKILIZA GNAKO AKIMZUNGUMZIA JOHN B CLICK HAPA
Ikumbukwe kuwa hii ni ngoma ya Pili kwa John B kutwangisha Collabo Wasanii kibao kwenye ngoma moja ambapo ya kwanza ilikuwa Ile WAZI ambayo iliwakutanisha Wasanii wa Tanzania, Kenya, South Africa na Nchi nyinginezo.

HABARI NA DJ HAAZU WA MAMBO JAMBO RADIO ARUSHA 93.0 FM

No comments: