22.11.13

Monday, August 19, 2013

(News) Wanawake wapokea Mikopo ya MWEI - Tegeta

 Bi. Prisca George (kulia) mkazi kutoka Tegeta, Dar es Salaam, anahesabu kitita cha mpoko alichopokea kupitia mradi wa MWEI unaoendeshwa na kampuni ya Vodacom Tanzania. Bi. Prisca ni mmoja wa wanawake wajasiliamali 150 waliopokea mikopo isiyo na riba ya jumla ya millioni kumi kupitia mradi wa MWEI eneo ya Tegeta ili kuendesha biashara zao. Kulia ni Bi. Grace Lyon, Meneja wa Mradi wa MWEI na katikati ni Bi. Zawadi Bakari, wakala wa M-Pesa. 

 Bi Zaituni Abdalla (kushoto) mkazi kutoka Tegeta, Dar es Salaam, anahesabu kitita cha mpoko alichopokea kupitia mradi wa MWEI unaoendeshwa na kampuni ya Vodacom Tanzania. Bi. Zaituni ni mmoja wa wanawake wajasiliamali 150 waliopokea mikopo isiyo na riba ya jumla ya millioni kumi kupitia mradi wa MWEI eneo ya Tegeta ili kuendesha biashara zao. Anayeshuhudia ni Bi Rukia Mtingwa, Meneja Mawasiliano Vodacom Tanzania. 

 Bw. Martin Kiswaga (kulia) ofisa kutoka kampuni ya Vodacom Tanzania, akielezea kikundi cha wanawake wajasiliamali kutoka Tegeta, Dar es Salaam, jinsi chaja ya ReadySet inavyofanya kazi. Chaja hio ilizinduliwa na kampuni ya Vodacom na inatumia nishati ya jua kuchaji simu kumi wakati mmoja. Wanawake hao pia walipata mikopo isiyo na riba kupitia mradi wa MWEI ya ujumla ya million kumi.  

No comments: