Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa,
akikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa duka la huduma kwa wateja la
Vodacom lililoko Msimbazi kariakoo
jijini Dar es Salaam. Pamoja nae katika picha ni Ofisa Mkuu
wa Mauzo na Usambazaji wa Vodacom Tanzania, Hassan Saleh kulia na Mkurugenzi wa Planetell David Hayes. Hilo ni duka la 70
la kampuni hiyo nchini.
Ofisa Mkuu
wa Mauzo na Usambazaji wa Vodacom Tanzania, Hassan Saleh, akimfafanulia
jambo Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa kuhusu mfumo wa uhifadhi wa taarifa
za M-pesa zinazowahusu wateja wakati Meya akiangalia huduma mbalimbali
zinazotolewa kwenye duka jipya la Vodacom Msimbazi mara baada ya
kulizindua.Wengine pichani ni Meneja wa duka hilo Josephine Swai na Mkuu wa
kitengo cha Mauzo wa Vodacom
Ofisa Mkuu
wa Mauzo na Usambazaji wa Vodacom Tanzania, Hassan Saleh, akifafanua
jambo kwa Mstahiki Meya wa manispaa ya Ilala Jerry Silaa baada ya uzinduzi wa
duka jipya la huduma kwa wateja la Vodacom lililoko Msimbazi karikoo jijini Dar
es Salaaa. Pamoja nao kutoka kushoto ni
Meneja wa duka hilo Josephine Swai na Mkuu wa kitengo cha Mauzo wa kampuni
hiyo Upendo Richard. Kampuni hiyo imefikisha maduka 70 ya huduma kwa wateja nchini.
Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa (kulia),
akisalimiana na Mkurugenzi wa Pantell David Hayes wakati akiwasili kwa ajili ya ufunguzi
wa Duka jipya la Vodacom lililoko
Msimbazi kariakoo jijini Dar es Salaam, Wanaoshuhudia wa kwanza kushoto ni Mkuu wa kitengo cha Mauzo wa kampuni
hiyo Upendo Richard, Ofisa Mkuu wa Mauzo na Usambazaji wa Vodacom Tanzania,
Hassan Saleh na Meneja uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim.
Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa,
akisikiliza maelezo kutoka kwa Mfanyakazi wa wa duka jipya la Vodacom Msimbazi namna
huduma zinavyotolewa kwa wateja wa kampuni hiyo. Wa kwanza kulia ni Ofisa
Mkuu wa Mauzo na Usambazaji wa Vodacom
Tanzania, Hassan Saleh. Meya Silaa alilizundua rasmi duka hilo.
Ofisa Mkuu
wa Mauzo na Usambazaji wa Vodacom Tanzania, Hassan Saleh, (wa kwanza
kushoto) akimueleza Meya wa manispaa ya
Ilala Jerry Silaa namna duka hilo linavyotoa huduma kwa wateja mara baada ya uzinduzi wa duka jipya la
huduma kwa wateja la Vodacom lililoko Msimbazi karikoo jijini Dar es
Salaaa. Pamoja nao katika ni Meneja wa
uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim, na Mkurugenzi wa Pantell David Hayes.
Dar es Salaam 17 Septemba 2013
. . . Ukuaji na uimarikaji wa
matumizi ya huduma za fedha mtandao nchini umekuwa wenye umuhimu mkubwa kwa
uchumi w anchi kwa hivio sasa ambapo kiasi kikubwa cha mzunguzko wa fedha za
shughuli za kiuchumi na kijamii zimekuwa zikitegemea huduma hizo na kuchangia
ukuaji wa uchumi.
Hayo
yamesemwa na Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa wakati wa uzinduzi wa duka
jipya la Vodacom Msimbazi jijini Dar es salaam ambapo alitumia fursa hityo
kusifu juhudi za Vodacom katika kuimarisha huduma zake ikiwemo ya M-pesa na
kuziletea karibu na wateja huduma zake zote.
Meya
Silaa amesema kwa kiasi mzunguko wa uchumi kwa sasa unategemea huduma za pesa
mtandao unaotumia teknolojia ya simu za mkononi ambapo huduma ya M-pesa imekuwa
ikiongoza soko huku akielezea jinsi ambavyo uwepo wa duka hilo kwenye eneo
ambalo ni kitovu cha biashara kwa nchi za maziwa makuu litakavyochangia uchumi
wa nchi na ustawi wa biashara.
"Hivi
sasa kuna matumizi makubwa ya huduma za fedha mtandao ambapo kila mmoja amekuwa
akitumia huduma hizo kwa ajili ya shughuli za kibiahara na kiuchumi huku
tukiona M-pesa inavyoongoza soko kwa hiyo tunaposhuhudia zuinduzi wa maduka
kama haya ni dhahiri kuwa tunaongeza matumizi ya huduma hizo."Alisema Meya
Silaa
"Msimbazi ni kitovu cha kikuu cha
baishara sio tu kwa Tanzania bali kwa nchi za maziwa makuu hivyo ni jambo
lisoepukika kuwa na maduka ya huduma kwa wateja ambayo yanafanya upatikanaji wa
huduma kuwarahisi na kwa kwa unafuu"
Hata
hivyo Meya Silaa amesema ukuaji wa baishara kwney sekta binafsi unatoa
changamoto kwa seriklai na halmashauri kuona ni jinsi gani mipango wanayoiweka
nayo pia iankwenda na kasi inayofanana.
"Miji
yetu inakuwa kwa kasi na wenzetu kwenye sekta binafsi wanavyoweka mikakati ya
kufikisha huduma zake karibu zaidi na wannachi tumesikia Vodacom wamefungua
duka Gongolamboto hii maana yake kwamba hata mipango yetu sisi nayo inahitaji
kuboreshwa penye Zahanati tuweke kituo cha afya huku tukipunguza
ukiritimba."
"Maduka haya yana mchango mkubwa kwa
kuwa mbali na kusogeza huduma karibu na
wananchi pia yanatengeneza ajira na kukuza biashara ambayo mwisho wa yote ni
ulipaji wa kodi ambazo zinakuja kuwa msaada kwa wananchi wote kwa ujumla."
Alisema Silaa na kuongeza "Hata hivyo usishnagae kwamba kibali tu cha
ukarabati wa jengo hili umechukua mwezi mzima haya ni ammbo ambayo hayakubaliki
katika zama za sasa za baishara lazima tupunguze ukiritimba na kuweka mifumo
rahisi kwa biashara kwa kuwa zinachangia kwenye kodi."
Kwa
upande wake Ofisa Masoko Mkuu wa Mauzo na Usambazaji wa kampuni ya Vodacom
Hassan Saleh amesema mapema mwaka huu Vodacom ilijiwekea lengo la kufungua
maduka 100 ya huduma kwa wateja ikilenga kuziwezesha huduma zake kuzileta
karibu zaidi na wateja kuwawezesha kupata huduma hizo kwa urahisi na kwa
gharama nafuu.
Saleh
amasema ongezeko la wateja wa Vodacom na ukuaji wa miji nao unachangia kutoa
msukumo kwa lengo hilo na kwmaba duka la Msimbazi ni la 70 kwa Vodacom nchi
nzima na la 18 kwa mkoa wa Dar es salaam na kwamba kazi ya kufungua maduka hayo
inaendelea nchi nzima.
"Mwaka
huu tulijiweka lengo mahsusi la kupeleka huduma zetu karibu zaidi na wateja
wetu ikiwemo kufungua maduka haya katikakati ya miji na nje ya miji ili
kuwapunguzia usumbufu wateja wetu ambao wamekuwa wakilazimika wakati mwengine
kufuata huduma hizi kwenye maduka yetu ya mbali."Alisema
"Tunajisikia
furaha kubwa kuona tunakwenda vizuri na utekelezaji wa lengo letu, ahadi yetu
ni kuendelea kutoa huduma bora kwa wateja wetu na kwamba kazi hii ya ufunguzi
wa maduka inaendelea Dar es salaam na nje ya Dar es salaam."
Saleh
amewaomba wannachi kutumia fursa ya uwepo wa maduka hayo mapya karibu na makazi
ama shughuli za biashara ili kupata huduma zote za Vodacom na kwamba hakuna
ulazima wa wao kufuata huduma hizo kwenye maduka waliyoyazoea ya Mliamni City
na Samora.
"Kabla
ya maduka haya mapya wengi wa wateja wetu walikuwa wakifuata huduma kwenye
maduka machache yaliyokuwepo hii iliwasababishia gharama na usumbufu wa kupanga
foleni, hali hiyo kwa sasa haina tena ulazima na tutaendelea kuimaliza kadri
tunavyofungua maduka haya mapya." Alisema Saleh
Katika
maduka hayo, huduma zote za Vodacom zinapatikana ikiwemo ya usajili, utatuzi wa
matatizo ya kiufundi ikiwemo ya data, huduma za M-pesa na nyinginezo.
Mwisho……./////
No comments:
Post a Comment