Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya
ufundi Phillip Mulugo akifurahia jambo na Meneja Masoko wa Mikono Business Consult Bi. Nestoria Simon (kushoto)na
Mkuu wa kitengo cha Vodacom Foundation Bw.Yessaya Mwakifulefule mara baada ya
kuelimishwa kuhusu na matumizi bora ya
pedi kwa wanafunzi wakike waliopo mashuleni,alipofika katika uzinduzi wa maonesho
ya Vodacom Elimu Expo yaliyofanyika katika viwanja vya posta kijitonyama jijini
Dar es salaam.
Naibu Waziri
wa Elimu na Mafunzo ya ufundi Phillip Mulugo,akifafanuliwa jambo na Meneja masoko wa Vodacom M-PESA Bw.Nixon
Bonaventure,alipotembelea banda la kampuni hiyo mara baada ya kuzindua rasmi maonesho
ya Vodacom Elimu Expo yaliyofanyika kwa
siku tatu katika viwanja vya posta kijitonyama jijini Dar es salaam.
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya ufundi Phillip
Mulugo,akifafanuliwa jambo na Mkuu wa
Idara ya Masoko na Mawasiliano Bw.Kelvin Twissa kuhusu huduma mbalimbali
zinazotolewa na Vodacom hususani M-PESA
kwenye sekta ya Elimu nchini,alipofika katika viwanja vya posta kijitonyama
jijini Dar es salaam,kuzindua maonesho
ya Vodacom Elimu Expo yaliyofanyika kwa
siku tatu.
Mulugo
asisitiza ushiriki wa kila mtanzania katika kuendeleza elimu
Dar es Salaam, Naibu
waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Philipo Mulugo, amewaasa wazazi, walezi na
jamii kwa ujumla kutumia teknolojia ya elimu masafa na mitandao kwa kupata
taarifa za uhakika za kitaluma na kimaendeleo.
Akizungumza wakati wa
uzinduzi wa maonesho ya Vodacom Elimu Expo 2013 juzi, jijini Dar es Dalaam, Waziri
Mulugo alisisitiza kuwa ushiriki wa wandau wote kuendeleza sekta ya elimu
inafungua fursa ya kupata na kutoa elimu bora kwa kila mtanzania.
Maonesho ya Vodacom Elimu Expo 2013 ni ya kwanza Tanzania
yaliodhaminiwa na kampuni ya simu ya Vodacom kupitia huduma yake ya M-Pesa
inayowezesha malipo ya karo ya shule kwa urahisi zaidi.
Waziri Mulungo alisema: ““Hii ni fursa kubwa sana kwa wote
wanaoshiriki maonesho haya ususani wanafunzi, walimu na wazazi. Yanatoa nafasi
kwa kila mdau wa elimu kuchangia maendeleo ya elimu nchini. Na hasa ukizingatia
kukuwa kwa matumizi ya mtanda na simu za mkononi katika kila kaya, ni fursa
kubwa katika kubadilishana mawazo ya kujenga Tanzania yenye elimu bora na
shindani katika Nyanja za kimataifa.”
Alidokeza kuwa Serikali kupitia wizara ya elimu, ipo katika
hatua za mwisho za kutengeneza mkongo wa taifa utakao unganisha upatikanaji wa
mtandao nchi nzima kapitia program ijulikanayo kama ‘Tanzania Beyond Tomorrow’ kwa
kushirikiana na makampuni ya mawasiliano katika kuboresha elimu masafa yaani”e-learning”.
“Naipongeza kampuni ya Vodacom kwa kuwa kampuni ya kwanza nchini kushirikiana na Serikali kutekeleza
mpango huu katika kuhakikisha kuwa sekta ya elimu inaendelea na kuwa bora zaidi.
Sasa ni rahisi kwetu wazazi kutumia njia bora, tena ya uhakika naya kuhaminika
ya M-Pesa kulipia watoto wetu karo ya shule,” alisema Mulugo.
Naye Robert Mihalo, ambaye ni mwanafuzi wa shule ya green
acres ya jijini alipongeza wadhamini na waandaji wa maonyesho hayo akisema:
“Nimeweza kubandilishana mawazo na wanafunzi wa shule zingine. Zaidi ya yote,
nimepata mbinu mpya kwa kupanua wigo wa ushiriki wa wanafunzi katika kuleta
elimu bora Tanzania.”
Maonesho haya ni muhimu sana kwani
yanawaelimisha wananchi kuhusiana na Vodacom Elimu Expo 2013 ambayo itaaanza
kutoa taarifa muhimu zinazohusu shule mbalimbali ikiwa ni pamoja na gharama za
ada na michango mingine katika shule husika.Aidha itaendelea kutoa taarifa
zinazohusu vyuo na taasisi za elimu ya juu ikiwa pamoja na fani zitolewazo
katika vyuo husika pamoja na gharama zake kupitia simu za viganjani,tovuti na
blogs za elimu.
Nae Mkuu wa Idara
ya Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Kelvin Twissa,ambao ni wadhamini wakuu wa
maonesho hayo alionyesha matumaini yake
kwa maonesho hayo na kusema kampuni yake inaelewa umuhimu wa elimu kwa kila mtoto
kwa hiyo wanajisikia fahari kudhamini maonesho hayo kwani yanalenga kuboresha
elimu ya Tanzania.
Wadhamini
wengine wa Maonesho hayo ni :- Clouds FM, DTV, Entertainment
Masters, Maxmalipo, Times FM, Primebiz Solutions Ltd na bima ya taifa ya afya, NSSF,
Azania Bank, FNB, Primebiz, NHIF, IPS, NMB, Global publishers, DSTV, Clouds FM.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment