Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Tanzania,Bw.Salum Mwalim akiongea na
waandishi wa habari(hawapo pichani) wakati wa hafla fupi ya kukabidhi
katoni hamsini za maji na fulana 1,000 kutoka Vodacom kusaidia matembezi
ya hisani yanayofanyika kesho Jumamosi 12 Oktoba, 2013 jijini Dar es
salaam kuleta hamasa kwa wananchi kuchangia kampeni ya kumaliza uhaba wa
madawati katika Manispaa ya Ilala. Kushoto ni Mstahiki Meya wa Manispaa
hiyo Jerry Silaa aliyendaa matembezi hayo.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa akiongea na waandishi wa
habari(hawapo pichani) wakati wa hafla fupi ya kupokea katoni hamsini za
maji na fulana 1,000 kutoka Vodacom kusaidia matembezi ya hisani
yanayofanyika kesho (Jumamosi 12 Oktoba, 2013) jijini Dar es salaam
kuibua hamasa kwa wananchi kuchangia kampeni ya kumaliza uhaba wa
madawati katika Manispaa ya Ilala. Kulia ni Meneja Uhusiano wa Nje wa
Vodacom Tanzania,Bw. Salum Mwalim
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa (wa pili kushoto) na
Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim wakionesha kwa waandishi
wa habari fulana zilizotolewa na Vodacom kusaidia matembezi ya hisani
yanayofanyika kesho Jumamosi 12 Oktoba, 2013 kuibua hamasa kwa wananchi
kuchangia kampeni ya kumaliza uhaba wa madawati katika Manispaa ya
Ilala. Vodacom imetoa fulana 1,000 na maji katoni 50. Wengine pichani
ni Zainabu Katimba na Halima Bulembo wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es
salaam waliojitolea kusaidia usimamizi wa matembezi hayo.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa(wa pili kuhsoto) akipokea
kutoka kwa Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim sehemu ya
fulana 1,000 zilizotolewa na Vodacom kusaidia matembezi ya hisani ya
kuhamasisha jamii kuchangia kampeni ya kumaliza uhaba wa madawati katika
Manispaa ya Ilala. Wengine pichani ni Zainabu Katimba (kushoto) na
Halima Bulembo wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam waliojitolea
kusaidia usimamizi wa matembezi hayo.
No comments:
Post a Comment