22.11.13

Wednesday, October 23, 2013

(News) BENKI YA KCB YAENDELEZA KAMPENI YAKE YA KUGAWA MADAWATI NA MITI SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI

 Baadhi ya wanafunzi wa shule ya Msingi Sinza Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam,wakifundishwa jinsi ya kuandika mwandiko mzuri na Ofisa kitengo cha mikopo wa  Benki ya KCB Tanzania, Bw. Innocent Mlimuka walipofika shuleni hapo kutoa msaada wa madawati 100 shuleni hapo.

 Mwalimu Venancia Venant (watatu toka kushoto waliokaa) wa shule ya Msingi Makumbusho Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam,akisikiliza jambo toka kwa Ofisa wa kitengo cha mikopo wa  Benki ya KCB Tanzania, Bw. Innocent Mlimuka mara baada ya kukabidhiwa msaada wa madawati 100 kutoka benki hiyo kwaajili ya matumizi ya wanafunzi wa shuleni hiyo.

 Baadhi ya wanafunzi wa shule ya Msingi Sinza Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, wakimsikiliza Meneja Uhusiano wa Umma wa benki ya KCB Tanzania, Bi. Hellen Siria alivyokuwa akiwaelezea umuhimu wa Elimu na kutunza madawati 100 waliyopewa msaada na benki hiyo kwa manufaa ya wanafunzi wengine.

Afisa Elimu kata ya Msasani,Bw.Kebero Maulid,akipanda mti katika shule ya Msingi Mbuyuni iliyopo Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam,Jumla ya  miti Elfu mbili na Madawati 100 yalitolewa msaada na Benki ya KCB Tanzania kwa ajili ya shule za msingi 6 na sekondari moja ya oysterbay zote za Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam,anaeshuhudia kulia ni Mwfanyakazi wa benki hiyo,Bw.Tito Mbise.

No comments: