22.11.13

Thursday, October 17, 2013

(News) DJ CHOKA kuwapa 'DEAL' wasichana 3 wanaojua kurap vizuri.

Member wa B Hitz Music Group Dj Choka ambae anafanya project za Hip Hop kwa kuwaunganisha wasanii wenye uwezo mkubwa wa kurap, na kuwaweka kwenye wimbo mmoja, amesema anampango wa kuwapa deal hiyo pia wasichana watatu wanaojua kurap vizuri lakini hawajatoka.
 Dj Choka ameiambia tovuti ya Times FM exclusively kuwa ameona kwenye ngoma zake wanahitajika wasichana wengine wanaoweza kuchana, huku akipigia mstari uwezo wa wasichana hao(wawe wakali).

 “Nafikiria tena kufanya ngoma na wasichana wanaorap lakini wakali, yaani nataka nikipata wawili lakini wawe wanarap ile yenyewe yani, haijalishi Kiswahili au kiingereza. Unajua kwenye ngoma zangu mi naona namuweka tu Vanessa Mdee, unajua Vanessa anaimba lakini akija kwenye project yangu inabidi achane.” Amesema Dj Choka.

Kuhusu sifa na jinsi ya kuwapata wasichana hao, alifunguka, “nafikiria kufanya Ki-search kidogo hivi lakini ntawaambia kwa kuwa bado ni mapema, nataka kufanya search ndogo tu ili nipate wasichana kama watatu hivi ambao watakuwa wanarap,ntafanya search siku si nyingi tu halafu ntawapata hao, kwa hiyo wakae mkao wa kula .”

Dj Choka hivi sasa anapika project yake anayofanya na wasanii kadhaa wenye umri mdogo na tayari Young Dee, M-Rap, Janjaro na Country Boy wameshaweka vocal ndani ya studio za BHitz, lakini Dj amesema zipo project nyingine zitakazotangulia kutoka kabla ya project hiyo.

Source: TIMES FM

No comments: