Baada ya kuwafahamu majaji wawili wa
TPF6 ambao ni Ian Mbugua (Kenya) na Juliana Kanyomozi (Uganda), hatimaye
jina la jaji wa tatu limefahamika ambapo C.E.O wa BHitz Music, Hermes
Bariki a.k.a Hermy B (Tanzania) ndiye atakayeungana na majaji hao
wawili.
Akiongea na 100.5 Times fm Hermy B
amewashauri watanzania kuwasapoti washiriki wanne kutoka Tanzania kwa
kuwapigia kura kwa kuwa ushindi hutokana na wingi wa kura anazopigiwa
mshiriki na sio anachosema jaji.
“Watanzania wasifikirie kwamba Jaji wao
ndiye atakayewapatia ushindi washiriki wao, ndio wapige kura sasa, kwa
sababu ushindi wa watu wengi unatokana na kura na sio jaji, hata Juliana
akimwambia you are the best of the best lakini asipopigiwa kura hawezi
kushinda.” Amesema Hermy B.
Washiriki watakaoiwakilisha Tanzania katika TPF6 ni Angella Karashani a.k.a Angel, Tanah, Hisia na Dubson.
Mshindi wa mwaka huu atapewa shilling
Million Mia Moja, na mkataba wa kurekodi nyimbo kwa gharama ya shilingi
Million mia mbili za Tanzania.
Source: XDeejayz
No comments:
Post a Comment