Nahodha wa timu ya soka ya Wahariri nchini Kulwa Karedia akiongea na
waandihsi wa habari(hawapo pichani)muda mfupi kabla ya kupokea vifaa
mbalimbali vya michezo kwa ajili ya timu yake na ya wanahabari wa mkoa
wa Iringa vyenye thamani
ya Sh 3 Milioni. Timu mbili hizo zinakutana kwenye mechi ya kirafiki
itakayochezwa mjini Iringa mwishoni mwa wiki.Kulia ni Meneja Uhusiano wa
Nje wa Vodacom Salum Mwalim na kushoto ni Meneja Uhusiano wa Umma wa
kampuni hiyo Matina Nkurlu.
Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim akikabidhi kwa Nahodha wa
Timu ya Soka ya Wahariri Kulwa Karedia vifaa mbalimbali vya michezo kwa
ajili ya timu yake na ya wanahabari wa mkoa wa Iringa vyenye thamani ya
Sh 3 Milioni.
Timu mbili hizo zinakutana kwenye mechi ya kirafiki itakayochezwa mjini
Iringa mwishoni mwa wiki.Wanaoshuhudia ni Meneja Uhusiano wa Umma wa
Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu(wa kwanza kushoto) na Nahodha Msaidizi
Saleh Mohammed
Kutoka Kulia Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim, Nahodha
Msaidizi wa Timu ya Soka ya Wahariri Saleh Mohamed, Nahodha wa timu hiyo
Kulwa Karedia na Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania,Matina
Nkurlu wakionesha sehemu
ya vifaa mbalimbali vya michezo vilivyotolewa na Vodacom kuwezesha
mechi kati ya timu ya Wahariri na Timu ya wanahabari wa Mkoa wa Iringa.
Mechi hiyo itachezwa mwishoni mwa wiki mjini Iringa.
Timu
ya soka ya Jukwaa la Wahariri Nchini – TEF na ile ya Wanahabari wa Mkoa
wa Iringa leo zimepokea vifaa mbalimbali vya michezo kwa ajili ya
mchezo wao wa kirafiki utakaochezwa mwishoni mwa wiki mjini Iringa.
Vifaa
vilivyokabidhiwa leo na Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Tanzania
Salum Mwalim kwa Nahodha wa timu ya Wahariri ambae pia ni Mhariri Mkuu
wa Habari wa Gazeti la Mtanzania Kulwa Karedia ni pamoja na jezi seti
tatu, viatu, mipira, suti za michezo na soksi.
Akikabidhi
vifaa hivyo leo jijini Dar es salaam, Mwalim amesema ni matokeo ya
Vodacom kutambua umuhimu wa michezo na namna ambavyo Wahariri
wanavyohitaji
muda wa kushiriki michezo kwa afya na burudani kutokana na uasili wa
majukumu yao ya kila siku.
“Tunafahamu
jinsi kazi za Wahariri zilivyo hivyo hii ni fursa nzuri kwao kufanya
jambo tofauti ili waweze kuwa na Wakati wa kuburudisha akili nje
ya maeneo yao ya kazi tunaamini ni tukio zuri na muhimu kwao”Alisema
Mwalim
“Wanahabari
wamekuwa wadau wetu wakuu katika biashara hasa pale tunapohitaji
kuupasha umma juu ya shughuli zetu mbalimbali hivyo nasi leo tunajisikia
furaha kuwezesha tukio lao.” Aliongeza
Mwalim
amesema Vodacom inatambua umuhimu wa michezo na ndio maana imekuwa mdau
mkubwa wa kuchangia maendeleo ya sekta hiyo hapa nchini kwenye ngazi
mbalimbali kuanzia ligi kuu hadi michezo ya ngazi za chini..
Kwa
upande wake Karedia ameishukuru kampuni hiyo kwa kuiwezesha mechi hiyo
jambo ambalo linaonesha jinsi kampuni hiyo ilivyo karibu na wanahabari
nchini.
“Tunategemea
kupata ushindani mkubwa kutoka kwa wanahabari wa mkoa wa Iringa nasi
katika kuhakikisha tunatimzia azima ya ushindi timu yangu imekuwa
kwenye mazoezi na tunaahidi kubeba zawadi ya ushindi.”Aliongeza
“Tunayofuraha
kubwa sana kuona Vodacom ikituunga mkono kutuwezesha mechi yetu
ikifana,vifaa hivi tunavipokea kwa furaha na tunaahidi kurudi na
ushindi.”Alisema Karedia
Amesema maandalizi ya mechi hiyo yamekamalika na kwamba itafunguliwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Dkt.Christine Ishengoma
Mbali
ya kuzipatia vifaa timu zote mbili, Vodacom imetoa pia seti moja ya
jezi na mipira minne kwa ajili ya zawadi ya mshindi wa mechi hiyo.
Mbali
ya kuidhamini mechi hiyo, Kampuni ya Vodacom imechangia pia Shilingi 12
Milioni kwenye maandalizi ya Mkutano Mkuu huo wa TEF uliopangwa
kufanyika
kwa siku mbili Oktoba 25 na 26 Mjini Iringa.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment