Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasilino wa
Vodacom Tanzania Kelvin Twissa, akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari wakati wa kutangaza
ujio wa wasanii wa Muziki wa kizazi kipya Peter na Paul Okoye maarufu kama P – square
kutoka nchini Nigeria chini ya udhamini wa Vodacom Tarehe 23 Mwezi ujao. Wasanii hao
wataambatana na wasanii wengine 13 kutoka nchini humo. Pamoja nae katika picha
ni Mtangazaji wa East Afrika Radio, Hillary Daudi (Zembwela).
Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasilino wa Vodacom Tanzania
Kelvin Twissa, akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kutangaza ujio wa
wasanii wa Muziki wa kizazi kipya Peter na Paul Okoye maarufu kama P – square
kutoka nchini Nigeria chini ya udhamini wa Vodacom, watakaowasili Tarehe
23 Mwezi ujao. Wasanii hao wataambatana na wasanii wengine 13 kutoka nchini
humo. Pamoja nae katika picha ni Mtangazaji wa East Afrika Radio, Hillary Daudi
(Zembwela).
Mtangazaji wa East Afrika Radio, Hillary Daudi
(Zembwela)akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kutangaza ujio wa
wasanii wa muziki wa kizazi kipya Peter na Paul Okoye maarufu kama P – Square
kutoka nchini Nigeria pamoja na mdhamini Mkuu,Tarehe 23 Mwezi ujao ndipo
watawasili nchini. Wasanii hao wataambatana na wasanii wengine 13 kutoka nchini
humo. Pamoja nae katika Picha ni Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasilino wa
Vodacom Tanzania Kelvin Twissa ambo ndio wadhamini wa onesho hilo.
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia
kwa makini maelezo kutoka kwa wazungumzaji Mtangazaji wa East Afrika Radio,
Hillary Daudi (Zembwela). Na Mkuu wa
Kitengo cha Masoko na Mawasilino wa Vodacom Tanzania Kelvin Twissa , wakati wa
Kutangaza ujio wa wasanii wa Muziki wa
kizazi kipya Peter na Paul Okoye maarufu kama
P – square kutoka nchini Nigeria, Tarehe 23 Mwezi ujao. Wasanii hao
wataambatana na wasanii wengine 13 kutoka nchini humo.
Dar
es Salaam 10 Oktoba 2013 ……
Kama ni siku ambayo inasubiriwa kwa hamu na wapenzi wa muziki basi ni Novemba
23 ambapo wasanii Mapacha Petter na Paul Okoye,wanaojulikana kama “P – Square”
watatoa burudani ya karne katika viwanja vya leaders Club jijini Dar es Salaam
chini ya udhamini wa Vodacom Tanzania.
Wasanii hao kutoka
nchini Nigeria kwa sasa wanatamba na kibao chao cha Personally wameendelea
kukonga nyoyo za wapenda burudani ndani na nje ya bara la Afrika huku matamasha
yao yakivutia mamia ya mashabiki na kupata mapokezi makubwa kila wanafanya
tamasha.
Akizungumza katika
mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika Hoteli ya Hyatt jijini Dar, Hillary
Daudi wa East Afrika Radio, Amesema onesho hilo litakuwa la kipekee. P- Square
wataongozana na wasanii wengine 13 ambao watatoa burudani ya Live Band siku
hiyo. Pamoja na wasanii wengine kutoka Tanzania.
“Wote tunatambua
namna kundi hili linavyofanya vizuri ndani na nje ya bara la Afrika, licha ya
kutoa burudani kwa mashabiki, pia litatoa fursa kwa wasanii wa ndani kujifunza
kutoka kwa wasanii hawa vijana ambao wamepata mafanikio makubwa kutokana na
kazi yao ya muziki,” alisema na kuongeza “hii itakuwa ni fursa ya kipekee kwa
wasanii wetu wa bongo kujifunza kwa kuangalia wenzao wanavyofanya kazi”.
Kwa upande wake Mkuu
wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Kelvin Twissa, ambao
ndio wadhamini wakuu wa onesho hilo amesema Vodacom inafurahi kuendelea kuwa
sehemu ya kutoa burudani kwa jamii ya Watanzania na safari hii ikiwaleta
wasanii ambao ni kipenzi cha Watanzania wengi.
“Siku zote Vodacom
imeendelea kuwa chaguo la kwanza kwa Watanzania, kuanzia katika burudani na
hata huduma nyingine za mawasiliano na kijamii. Tunaendelea kuunga jitihada za
kuwainua wasanii wetu wa ndani kwa kuwapatia fursa ya kujifunza kutoka kwa
wasanii wenzao wakubwa waliofanyikiwa
kufanya kazi zao Kimataifa.” Alisema Twissa na kuongeza
“Kwa wateja wa
Vodacom ambao pia ni mashabiki wa wasanii hawa ambao wanatamba na kibao chao
kitamu cha ‘Personally’ kwa sasa wanayo fursa ya kufurahia nyimbo hizi kwa
kuzidownload au kuzitumia kama miito ya simu (RBT) na kuweza kujishindia tiketi
za onesho hilo. Natoa wito kwa Watanzania wapenda burudani kutembelea ukurasa
wetu wa Facebook na Twitter kwa taarifa zaidi na kujua namna ya kujishindia
tiketi za onesho hilo.
Tamasha hilo linalo
ratibiwa na East Afrika Radio na TV na kudhaminiwa na kampuni ya Vodacom
Tanzania Linatarajiwa kuwa la kihistoria katika burudani ya muziki wa kizazi kipya nchini.
MWISHO.
MWISHO.
No comments:
Post a Comment