22.11.13

Saturday, October 12, 2013

(News) Video ya Touch iko tayari, the video is nice na sitawaangusha "WAKAZI"

Rapper mwenye uwezo mkubwa wa kutumia lugha mbili ‘bilingual’ Webiro N. Wasira maarufu kama Wakazi amesema video ya wimbo wake ‘Touch’ iko tayari na anajiandaa kuiachia ili watu waweze kuiona akianza na watu wake wa karibu na wadau wa media.
Wakazi amefunguka katika kipindi cha ‘The Chat’ cha 100.5 Timesfm kinachoendeshwa na Ezden Jumanne a.k.a Ezden The Rocker Jumamosi saa nne kamili asubuhi hadi sita kamili mchana.
 “Ebana video ya Touch iko tayari na maandalilzi yako fresh, editing na kila kitu kimeshafanyika so kilichobaki hapa sasa hivi naandaa just like planning kuhakikisha kwamba nairelease proper watu waweze kuiona ili. Mostly watakuwa watu wa media, watu wa radio, television, watu wa newspapers na blogers na watu wengine wa karibu waweze kuiangalia halafu baada ya hapo tutaiweka online and then tutaipeka kwenye different media as well,  kuhakikisha tunai-premier huko pia.”

Wakazi ameielezea kwa ufupi video yake kuwa ni video nzuri na kwamba kazi waliyoifanya ni kubwa na kwamba hatawaangusha fans wake. “ The video is nice and I’m happy kwa sababu tulifanya kazi ya ziada and the song is doing well and shout out to Timesfm kupitia ‘The Chat’, na watu wote wanaousikiliza wimbo na kuupenda pia.

Source: TimesFM

No comments: