Vodacom
yatunisha mfuko wa serikali
· Yalipa kodi ya Bilioni 29.2 ndani ya
miezi 6
·
Ni zaidi ya asilimia 86% ya mwaka uliopita
Dar
es Salaam: Ikiwa ni miezi sita tu
tangu kuanza kwa mwaka wa biashara unaoanzia tarehe 1 Aprili 2013, kampuni ya
Vodacom Tanzania imetangaza kulipa kodi ya kampuni ya shilingi bilioni 29.2/=
kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania, TRA.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi
Mtendaji wa Kampuni hiyo, Rene Meza, amesema, malipo ya kodi hiyo ni asilimia
86% ya malipo ya mwaka wa fedha wa 2012 ambapo kampuni hiyo ililipa Bilioni
15.7 kwa kipindi cha nusu mwaka.
“Tutaendelea kuwekeza katika Upanuzi na
Uboreshaji wa wa mtandao wetu, Kufikia sasa tuna zaidi ya minara 2700 nchini
kote ambayo inatoa huduma ya mawasiliano kwa zaidi ya asilimia 90% ya
Watanzania wote,” alisema Meza na Kuongeza, “ Pamoja na hayo tunaendelea
kujivunia mafanikio makubwa tuliyoyapata kwa kubadilisha maisha ya zaidi ya
Watanzania milioni 5 ambao wamechagua M pesa kuwa sehemu ya mfumo wa maisha yao
katika upataji wa huduma za kifedha. Kupitia huduma hii tumetengeneza ajira
zaidi ya elfu hamsini na kuwa sehemu muhimu katika kujenga uchumi wan nchi,”
alisema Meza.
Aidha Meza ametanabaisha
kuwa matumizi ya teknolojia bado yameendelea kuwa changamoto kwa watanzania akifafanua
kuwa matumizi ya Intaneti nchini kwa sasa ni asilimia 10% tu ukilinganisha na
asilimia 40 nchini Kenya huku akitoa wito kwa wadau wa sekta ya mawasiliano na
serikali kushirikiana katika kuweka mipango thabiti na kuendelea kuleta
mapinduzi ya kiteknolojia ili kuongeza matumizi ya intaneti kwa Watanzania
katika kupata taarifa mbalimbali.
Meza alienda mbali zaidi na
kusema kuwa Ongezeko la kodi kwa kampuni za simu litaathiri kwa kiasi kikubwa
maendeleo ya sekta hiyo katika upanuaji wa huduma na uendelezaji wa teknolojia
mpya kukwama kwa sababu huduma hiyo itakuwa ghari na Watanania wengi
watashindwa kuimudu, Pia itakuwa ngumu kwa kampuni kuendelea na ukuzaji na
uboreshaji wa miundombinu na kuleta teknolojia mpya.
“Kodi ya laini ya simu ya
Shilingi 1000/= kila mwezi itaendelea kuwa kikwazo kikubwa katika ukuzaji wa
sekta ya mawasiliano, ikiwa ni pamoja na upanuaji wa huduma za mawasiliano
maeneo ya vijijini, na itaendelea kuifanya huduma ya mawasiliano kuwa ghari na
kuhindwa kutumiwa na Watanzania wengi wenye kipato cha chini, alisema Meza na
kuongeza, “Itakuwa vigumu kuendelea kupanua huduma zetu katika maeneo ya
vijijini kama hakuna soko la wateja kwa sababu wengi watashindwa kutumia huduma
za mawasiliano,”
Kwa upande wao wachambuzi wa
sekta ya Mawasiliano wanasema kufungiwa laini kwa wateja watakaoshindwa kulipa
kodi hiyo ya shilingi 1000 ya kila Mwezi itapunguza pato la serikali kwa sababu
wateja wengi hao wanalipa asilimia 14.5% ya matumizi na asilimia 18% ya VAT kwa
matumizi hayo madogo ya kila siku.
Meza alihitimisha kwa kusema
kuwa Vodacom Tanzania imeendelea kuwa kampuni pekee na inayoongoza kwa kuwekeza
kwa kiasi kikubwa katika huduma za jamii ambapo kwa Mwaka 2012 kampuni hiyo
kupitia kitengo chake cha huduma za jamii cha Vodacom Foundation ilitumia
shilingi bilioni 11, katika kuendeleza sekta ya Afya, Elimu na miradi
mbalimbali ya kukuza uchumi kwa wanawake nchini ikiwa ni kiwango kikubwa
kutengwa na kampuni katika utoaji na uungaji mkono wa huduma za kijamii.
“Vodacom Foundation
imewezesha miradi zaidi ya 120 hadi sasa, ikiwa ni pamoja na uchangishaji wa
fedha katika kupambana na kutokomeza ugonjwa wa Fistula nchini, kuboresha
miundombinu ya mashule mbalimbali, na Miradi ya kuwawezesha wajasiriamali
wadogo kiuchumi hasa wanawaske kupitia mradi wa mikopo isiyokuwa na riba wa
MWEI, na miradi ya kuwezesha upatikanaji wa maji katika maeneo yanayo kabiliwa
na changamoto hiyo” alihitimisha Meza.
Mwisho…....
No comments:
Post a Comment