22.11.13

Monday, November 11, 2013

(News) Mikoa ya Kaskazini yaongoza kutimka na boda boda

 Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Bw.Matina Nkurlu(kushoto)akiwa pamoja na Ofisa wa bodi ya michezo ya kubahatisha Bakari Abdallah,Ofisa huduma za ziada wa Vodacom Rashid Maggid huku Kaimu mkuu wa kanda ya Kaskazini wa Kampuni hiyo Bi.Assumpta Malongo wakihakiki mmoja ya namba ya simu ya  washindi wa Promosheni ya “Timka na BodaBoda” iliyofanyika katika kituo cha radio cha Sunrise mjini Arusha juzi.Jumla ya washindi(95)wamejishindia Bodaboda na(55)wamejinyakulia fedha taslimu.Ili kujiunga na Promosheni hiyo tuma neno Promo kwenda 15544.

 Baadhi ya washindi wa Promosheni ya “Timka na BodaBoda”inayoendeshwa na Vodacom Tanzania wa mkoa wa Arusha na Kilimanjaro wakiondoka na Bodaboda zao baada ya kukabidhiwa rasmi jana jijini humo.Jumla ya washindi(95)wamejishindia Bodaboda na(55)wamejinyakulia fedha taslimu.Ili kujiunga na Promosheni hiyo tuma neno Promo kwenda 15544.

 Mshindi wa Promosheni ya”Timka na Bodaboda”inayoendeshwa na Vodacom Tanzania,Elinipa Mmari akinesha namba mpya ya pikipiki yake baada ya kukabidhiwa na Kaimu Mkuu wa kanda ya Kaskazini wa Kampuni hiyo Bi.Assumpta Malongo(kushoto)katikati ni mume wa mshindi huyo Alfred Mmari. Jumla ya washindi(95)wamejishindia Bodaboda na(55)wamejinyakulia fedha taslimu.Ili kujiunga na Promosheni hiyo tuma neno Promo kwenda 15544.

 Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Bw.Matina Nkurlu(kulia)akimfungia kamba ya kofia ngumu”Helmet”Mume wa mshindi wa Promosheni ya “Timka na BodaBoda mkazi wa Siha mkoani Kilimanjaro Alfred Mmari,kushoto ni  Kaimu Mkuu wa kanda ya Kaskazini wa Kampuni hiyo Bi.Assumpta Malongo(kushoto)katikati ni mume wa mshindi huyo Alfred Mmari. Jumla ya washindi(95)wamejishindia Bodaboda na(55)wamejinyakulia fedha taslimu.Ili kujiunga na Promosheni hiyo tuma neno Promo kwenda 15544.

 Kaimu Mkuu wa kanda ya Kaskazini wa Vodacom Tanzania Bi.Assumpta Malongo(kulia)akimkabidhi funguo ya pikipiki yake mshindi wa Promosheni ya”Timka na Bodaboda”Paulo Kivuyo mkazi wa njiro.Jumla ya washindi(95)wamejishindia Bodaboda na(55)wamejinyakulia fedha taslimu.Ili kujiunga na Promosheni hiyo tuma neno Promo kwenda 15544.

 Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Bw.Matina Nkurlu(kushoto)pamoja na Kaimu mkuu wa kanda ya Kaskazini wa Kampuni hiyo Bi.Assumpta Malongo,wakimshuhudia mshindi wa Promosheni ya”Timka na Bodaboda”Bw.Paulo Kivuyo wa Arusha akiwasha pikipiki yake mara baada ya kukabidhiwa rasmi jijini Arusha jana. Jumla ya washindi(95)wamejishindia Bodaboda na(55)wamejinyakulia fedha taslimu.Ili kujiunga na Promosheni hiyo tuma neno Promo kwenda 15544.

Kaimu mkuu wa kanda ya Kaskazini wa Vodacom Tanzania Bi.Assumpta Malongo,akimshuhudia  mshindi wa Promosheni ya”Timka na Bodaboda”Bi.Elinipa Mmari akiwa amepakizwa na mumewe Alfred Mmari  mara baada ya kukabidhiwa rasmi jijini Arusha jana. Jumla ya washindi(95)wamejishindia Bodaboda na(55)wamejinyakulia fedha taslimu.Ili kujiunga na Promosheni hiyo tuma neno Promo kwenda 15544.

Katika hali ya kushangaza wengi wakazi wa Arusha na mkoa wa Kilimanjaro, wanaoongoza kwa kuzoa Boda Boda nyingi katika promosheni ya Timka na Bodaboda inayoendeshwa na kampuni ya mawasiliano inayoongoza nchini Vodacom ambapo ikiwa ni siku 20 tu tangu kuanza kwa promosheni hiyo tayari jumla ya boda boda 29 zimenyakuliwa na wakazi wa mikoa hiyo.
Boda Boda hizo ambazo tayari zimepelekwa jijini humo kwa ajili ya kukabidhiwa kwa washindi zimeendelea kuvutia hisia za wakazi wa mikoa hiyo na kuzua gumzo kila upande juu ya washindi waliopatikana kutoka katika mkoa huo ambapo wengi waliamini kuwa Promosheni hizo hufanyika kwa Dar es Salaam tu.
Akizungumza wakati wa kuwakabidhi washindi pikipiki wa mikoa hiyo,Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania, Matina Nkurlu amesema wameshangazwa na ushindi mkubwa ambao wameupata wakazi wa kanda ya kaskazini .
“Watu wengi huwa wanaamini kuwa kila promosheni tunayoifanya huwa ni kwa wakazi wa Dar es Salaam tu hili si kweli kwani Wakazi wa Arusha na Kilimanjaro wamedhihirisha hili kwa kuutoa mkoa wao kimasomaso kwa kujizolea bodaboda 29 na bado ziko zaidi ya pikipiki hizo 370 ambazo zinaendelea kushindaniwa,” alisema Nkurlu na kuongeza.

“Tumeanza na wakazi wa Arusha na tutaenda pia katika mikoa mingine lengo letu sisi kama Vodacom ni kuhakikisha tunaendelea kuboresha na kuimarisha maisha ya wateja wetu ambao wamekuwa wakituunga mkono siku zote, Tunaamini kuwa kwa kuboresha maisha ya wateja wetu kutoka katika faida tunayoipata ili kuwawezesha wao kuendelea pia kutuunga mkono siku hadi siku na kwa nguvu zaidi,” alisema.
“Sasa hivi sehemu nyingi za Tanzania wakazi wengi wanapata tabu ya usafiri na usafiri rahisi kwa sasa ni pikipiki maarufu kama Bodaboda, gharama za maisha zimepanda sana usafiri pia umekuwa tabu, hivyo tumeona vyema sasa kuwapatia wateja wetu nafasi ya kujishindia usafiri ambao unatumia gharama nafuu,”
Nkurlu amesema jambo la msingi ni kuhakikisha tunawezesha ndoto za watanzania wengi kumiliki usafiri wao, na hata kwa wale ambao wanapenda kuwa wajasiriamali basi hii ni fursa ya kipekee kujishindia Bodaboda hizi.
Akizungumza baada ya kukabidhiwa zawadi ya bodaboda mume wa mshindi wa boda boda,Elinipa Mmari,Bw Alfred Mmari, alitoa wito kwa wanaume,kutowakataza  wake zao,kucheza bahati nasibu ya timka na boda boda kwani ina manufaa makubwa.
“mimi nilikuwa namkataza mke wangu, kucheza lakini baada ya ushindi huu,natoa wito kwa wanaume wenzangu kuwaacha wake zao kucheza na hata kuwasaidia kwani wanabahati ya ushindi”alisema Mmari
Katika hafla hiyo, iliyofanyika viwanja vya Sanawari,mfanyabiashara Paulo Lairumbe kivuyo,mkazi wa Njiro Arusha pia alikabidhiwa boda boda yake aliyeshinda.
Katika Promosheni hii ya Timka na Boda Boda kampuni ya Vodacom imetenga jumla ya bodaboda 430 kwa kipindi cha siku 100. Ili kupata nafasi za kujishindia bodaboda hizo, na shilingi milioni moja kila siku mteja wa Vodacom atatakiwa kutuma ujumbe wenye neno PROMO kwenda 15544.
Mwisho...

No comments: