22.11.13

Tuesday, August 28, 2012

Ten Years Later (Letter to Dandu)

Mambo vp! Jumatatu ya tarehe 27, August, 2012 ni miaka kumi tangu kifo cha marehemu James Maligisa Dandu aka "Mtoto wa Dandu" ama CJ Massive, aliyefariki kwa ajali ya gari jijini Dar es Salaam, August 27, 2002. J
> apo ni kama vile watu wameanza kumsahau lakini mimi sitoweza kumsahau kamwe. Aliniinspire sana kufanya muziki. So wiki hii mpaka ijumaa nimeamua niitumie kutafakari mazuri aliyoyafanya kwenye muziki wa Tanzania na nimemwandikia barua hii ambayo pia ina wimbo wake hapo kwenye attachment.
>
> Niaje Dandu, Sky hapa tena, nataka kuholla tena
> Last time nilikuwa Rock City, your home City
> This time nipo Dar city, the Hustles city
> August 27, 2002 with a fatal accident, shujaa ukawa umeaga
> Ten years later the game is still strong
> New Artists, new flows new production
> Rap bado ipo ila kiduku ndio fashion
> Wanauita muziki wa hela hawaaimbi kwa passion
> Muziki yes unalipa vijana wanadrive tu
> Gari za maana wachache wamestay true
> Show za laki laki humpati huyo Diamond
> Humpati AY humpati hata Saigon
> Clouds bado wapo watemi kama kawa
> Wanapiga tu mahela Fiesta kama dawa
> Bongo Records bado ipo ila P-Funk simwelewi
> Majani sio Majani, sio Kinywele kimoja tena
> Ameshalose focus MJ ye anapeta
> Piga sana mkwanja commercial mpaka noma
> BSS, matangazo Airtel mpaka Voda
> Mchizi yuko safi dread zake safi
> Vp maisha ya heaven? Hope it’s all good
> Dunia bado mbovu no money no food
> Somalia, Eritrea DR Congo
> Hakuna maisha bora shida tu hata Bongo
> CCM sio shwari this time wanaenda down
> CHADEMA wako hot wanaweza chukua hiyo crown
> Ufisadi bado upo wa Radar mpaka Dowans
> Story zile zile nightmare za Darwin
> Siasa na vijana inashika kwa kasi
> Sugu ndani ya mjengo alipata nafasi
> Zitto, January yule mtoto wa Makamba
> Mnyika, Tundu Lissu hawa jamaa wanatamba
> Kifupi Tanzania imeshachange sana man
> Thanks to the lord bado tunayo amani
> Ujinga na maradhi bado tatizo bado lipo
> Tumuombe Mungu tuje tuonane tena my brother

No comments: