22.11.13

Friday, August 24, 2012

Vodacom yapunguza gharama za matumizi ya intaneti kwa simu za Blackberry.

Taarifa kwa vyombo vya habari
Vodacom yapunguza gharama za matumizi ya intaneti kwa simu za Blackberry.
Dar es Salaam, 23, Agosti, 2012 … Wateja wanaotumia simu za Blackberry sasa watafurahia punguzo kubwa la gharama za matumizi kutokana na punguzo jpya la vifurushi vya Blackberry (BIS). Kampuni ya simu za Mkononi ya Vodacom imepunguza gharama mpya za matumizi ambazo zitawewezesha wateja kupata huduma za Blackberry kwa gharama nafuu kwa wiki na kwa mwezi.
Kwa wiki mteja atapata huduma za Blackberry kwa shilingi 6000/= pungufu ya gharama ya awali ya shilingi 7000, Huku mteja atakaejiunga kwa mwezi atalipia 17,500/= ikiwa ni punguzo kutoka gharama ya awali ya shilingi 20000/= mteja atanunua vifurushi kwa kupiga *149*01#.
Akizungumzia punguzo la vifurushi hivyo, Mkurugenzi mtendaji wa Kampuni ya Vodacom Tanzania Rene Meza, alisema kuwa vifurushi hivyo vitakuwa na faida kubwa kwa wateja wa Vodacom na kurahisisha matumizi ya kila siku ya intaneti kwa wateja.
Huduma ya intaneti ya Blackberry (BIS) inayojulikana pia kama ‘Blackberry Absolute’ inawawezesha wateja kupata huduma ya intaneti bila kikomo kwa zaidi ya akaunti nane za barua pepe, Kutuma ujumbe mfupi bila kikomo kupitia (BBM) Blackberry Messenger Service, huduma za ujumbe mfupi wa maneno kama Live Messenger, Google talk na Yahoo! Messenger, Blackberry AppWorld na Blackberry Shield, pamoja na huduma nyingine za taarifa na mawasiliano.
Vifurushi vipya vya huduma za Blackberry (BIS), vinatarajiwa kuongeza matumizi ya internet hususani kwa vijana ambao wanatumia intaneti kuperuzi na kupakua vitu mbalimbali.
Mwisho….//////

No comments: