22.11.13

Friday, March 08, 2013

Kundi jipya la kinadada la TRIO latoa wimbo mpya

Kina dada watatu kutoka Nyumba ya Vipaji Tanzania, The TRIO, wametoa wimbo wao mpya unaoitwa, ‘PAMBO’ ambao ni maalumu kwa ajili ya kuadhimisha siku ya wanawake duaniani.
Kundi hilo ambalo limekuwa kwenye muziki kwa muda mrefu kidogo, sasa wameamua kutoa wimbo huo ikiwa ni maandalizi ya ujio wao kamili mwishoni mwa mwezi huu.
Pamoja na wimbo huo, The TRIO pia wametoa video ya live performance ya wimbo wao wa ‘FALL IN LOVE’ ambayo ilirushwa kwa mara ya kwanza kwenye vituo vya luninga wakati wa sherehe za Valentine mwaka huu.
Kundi hilo linaundwa na kinadada watatu machachari, Angella Karashani (Malaika), Alice Kibopile (Alice) na Khadija Maige (Kadja)
Wimbo umerekodiwa studio ya Sourround Sound, chini ya mtayarishaji Ema The Boy.

No comments: