22.11.13

Wednesday, March 27, 2013

SIMULIZI YA KUSISIMUA,,, BADO MIMI SURA YA .......1......

“Napata  maumivu makali sana jamani naombeni mnisaidie nateseka sana eeh Mungu wangu” ilikuwa ni sauti ya  Mama kutoka chumbani niliinuka na kukimbilia ndani huku nikimwangalia Mama kwa huzuni kutokana na maumivu ya tumbo aliyokuwa akiyasikia nilisogea karibu “Pole mama twende nikupeleke Hospitali” Alijivuta kidogo na kuinua uso wake huku akinitazama “Mwanangu baba yako yuko wapi”  Nilimshika mama mkono “Baba ametoka ameenda kazini”.

 Kutokana na hali aliyokuwa nayo Mama nilitamani kumsaidia lakini sikuwa na namna kwani maumivu aliyokuwa anayapata yalikuwa makali sana “Kandida mwanangu naomba umtafute Baba yako anipeleke hospitalini” Baba yangu alikuwa ni mfanyakazi katika kiwanda cha plastiki na Mama alikuwa hana kazi nikiwa ni mtoto wa kwanza katika familia yetu na wadogo zangu wawili ambao wote walikuwa wakisoma shule ya msingi wakati huo mimi nilikuwa kidato cha pili pale nyumbani hakukuwa na mtu yeyote zaidi yangu na Mama alikuwa ni mgonjwa, hali ya mama yangu ilizidi kuwa mbaya ikanibidi nikimbie kwenda kumuita jirani yetu anayeitwa  Mama Keku.

2 comments:

ADELA KAVISHE said...

thanx a lot wangu pamoja sana

ADELA KAVISHE said...

mambo hope uko poa nimeweka muendelezo sura ya .....2.....