Mwenyekiti
wa TUMA nchini, Fredrick G Mariki (Mkoloni) ametoa salamu hizo za pole kwa
familia ya marehemu Mangwea, ndugu, jamaa, marafiki pamoja na mashabiki wa Bongo
Fleva waliopo ndani na nje ya nchi kutokana na kuondokewa kwa msanii maarufu
Albert Mangwair.
Marehemu
Albert Mangwea ambaye alikuwa nchini Afrika Kusini kwa shughuli za kimuziki
alifikwa na mauti hayo huku akiwa amelala katika chumba ambacho alikuwa na
rafiki yake aliyetambulika kwa jina la M to The P ambaye naye alikimbizwa
Hospitali ya St Helen iliyopo nchini Afrika Kusini kwa matibabu huku taarifa
kamili ya kilichosababisha kifo cha Mangwea kikiwa bado hakijajulikana mpaka
hapo Hospitali hiyo itakaposema.
“kwa niaba
ya wanachama wa TUMA na Watanzania wote kwa ujumla napenda kutoa salamu za pole
kwa familia ya marehemu Albert Mangwair kutokana na pigo hili kubwa na kwa
kweli tumepoteza msanii wa kizazi kipya ambaye Taifa lilikuwa likijivunia
kuwepo kwake na kazi zake” alisema Mkoloni.
Chama cha
TUMA kinaungana na Watanzania wote katika kipindi hiki kigumu na kinatoa
ushirikiano wa hali na mali kama ambavyo kimekuwa kikifanya hivyo katika mambo
mengine yanayohusu wasanii nchini.
Mkoloni
alimaliza kwa kusema kuwa “ni kweli tulimpenda lakini Mungu alimpenda zaidi na
kuongeza kuwa ni wakati mgumu na tunatakiwa kushirikiana kwa pamoja katika
kipindi hiki huku akitoa angalizo kwa watu wanaotaka kutumia fursa hii kwa
ajili ya maslahi yao binafsi.
No comments:
Post a Comment