22.11.13

Thursday, May 30, 2013

(News) WALAKA RASMI KUTOKA KWA QS MHONDA J ENTERTAINMENT KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSIANA NA TAMASHA LA TAREHE 01/06/2013 NA MSIBA WA MSANII ALBERT MANG’WEA.

KUHUSIANA NA KIFO CHA MSANII ALBERT MANG’WEA.

Kampuni ya QS MHONDA J ENTERTAINMENT tunatoa salumu zetu za rambi rambi kwa familia ya marehemu ALBERT MANG’WEA  ambaye tunatambua na kuthamini mchango wake katika tasnia ya muziki ambayo inakua kila kukicha hivyo baada ya kutafakari sana kwa kina uongozi wa kampuni ukaona itakuwa ni jambo jema kama tutaendelea na TAMASHA  la tarehe 01/06/2013 ili kuwapa mashabiki nafasi ya kuichangia familia ya marehemu katika siku hiyo ya tamasha ambako kutakuwa na kipindi maalumu siku hiyo ambako kila ambaye atafika atapa nafasi ya kuichangia familia ya marehemu na tunaamini hii itakuwa ni nafasi kwa wakazi wa Dar es salaam kutoa rambi rambi zao na kuifikia familia ya marehem kupitia mwakilishi wa familia ya marehemu na pia sisi kama kampuni tutatoa mkono wa rambi rambi katika siku hiyo hivyo basi tunaomba wadau wa burudani wajitokeze kwa wingi siku ya tarehe  01/06/2013 katika ukumbi wa DAR LIVE ili kuweza kumuombea na pia wasanii mbalimbali wataimba nyimbo za kuomboleza.

No comments: