22.11.13

Monday, September 02, 2013

(Audio) Rukkii ft. Christian Bella - Mimi na Wewe

Msanii Rukkii anayejulikana kama Sweetty Rukiah Mohamed au Rukiah Mohamed ameangusha bonge la ngoma inayoitwa ‘Mimi na Wewe’ featuring Christian Bella.
Akiongea baada ya kuachia hii ngoma, Christian Bella alisema alifurahi sana kufanya huu wimbo na yuko na uhakika ni wa hali ya kimataifa. Ngoma hii imefanyika chini ya producer KGT kutoka studio za G-Records.

Rukkii alionekana kwa mara ya kwanza kwenye runinga katika tamthilia ya ‘Mtazamo’ ambayo ilikuwa inarushwa hewani kwenye kituo cha televisheni cha Channel TEN.
Mwaka wa 2012 ulikuwa mwaka mzuri kwa Rukkii, alishiriki katika shindano la ‘Imba Cheza Vaa kama Rihanna’ liloandanliwa na Global Publishers/Dar Live akishindania shilingi millioni kumi. Baadaye, alicheza filamu ya ‘Thecla’ na ‘Lugha Mseto’ zilizozambaswa na kampuni ya Whatever Films Production na Pili pili Entertainment. Lugha Mseto ni movie ambayo umempa umaarufu sana nchini. Hii filamu inaonyeshwa kwenye mabasi ya mikoani na pia kipande chake kimesambaa Whatsapp.
Mapema 2013, Rukkii alikuwa signed chini ya music label ya FMA - Flave Music Afrika.
‘Nimefurahi sana kupata sehemu ya kukuza kipaji changu cha mziki na kutimiza ndoto zangu za kuwa msanii wa kike bora Tanzania, Afrika mashariki na Africa nzima kwa ujumla’ Rukkii amesema.

Video ya huu wimbo inakusudiwa kutoka mwisho wa September.
Twitter @sweettyrukkii      Facebook page - Sweetty Rukiah - Rukkii


Thanks for your support.

No comments: