22.11.13

Tuesday, February 14, 2012

NI ZAWADI YAKO KUTOKA KWETU..HAPPY VALENTINE DAY....FROM T.H.T

Nyimbo Hizi Zimewahi Kuimbwa Na Wanamuziki Tofauti Wa T.H.T Na Leo Hii Zinaletwa Tena Kwako Zikiwa Zimeimbwa Na Wanamuziki Tofauti Wa T.H.T, Itapatikana Albam Nzima Lakini Pia kwa Sasa Zinapatikana Kama Calltone katika Simu Yako, Hii Ni kwa Wateja Wa AIRTEL TZ NA TIGO TZ,L engo Kubwa Likiwa Ni Kukuburudisha Wewe Shabiki Yetu Mpendwa Katika Kipindi Hiki Cha Sikukuu Ya Wapendanao...NI ZAWADI YAKO KUTOKA KWETU.
Zawadi Maalum Kwa Mashabiki,wapenzi Na Wadau Wa Muziki Popote Mlipo,Tumeamua Kuwapatia Zawadi Hii Kwa ajili Ya Mapenzi Yetu Kwenu Na Kuthamini Mapenzi Yenu Kwetu.



(1) Bembelezwa Kama Inavyojulikana Wimbo Huu Toleo La Kwana Uliimbwa Na Barnaba Na Ndiye Mtunzi Wake....Hii Ya Sasa Imeimbwa Na Linah Maalum Kwa Mashabiki Wote Katika Sikukuu Hii Ya Wapendanao.
DOWNLOAD
 

(2) Daima Na Milele Hii Mtunzi Wake Ni Marlow Na Toleo La Kwanza Aliimba Marlow Pia......Hii Ya sasa Imeimbwa Na Zao Jipya  Katika Muziki Huu Anaitwa Ally NipisheNi Kijana Mpya Mwenye Kipaji Cha Kipekeee.

(3) Robo Saa Mtunzi Na liyeimba Toleo La Kwanza Ni Amini....Hii Ya Sasa Imeimbwa Alice Kibz Na Mwimbaji Mpya Ndiyo Kwanza Kamaliza Masomo Yake Ya uimbajiT.H.T amerudia wimbo ambao Unamvutia toka Ajaanza Kujifunza Kuimba..sauti Mpya Ya Kike Ni Zawadi Kwaajili Yako.
DOWNLOAD
  

(4) Lonly Wimbo Huu Ulitungwa Na Barnaba Toleo La Mwanzo Aliimba Linah......Huu Wa Sasa Umeimbwa Na Mtoto Mwenye Umri wa Miaka 13 Anaitwa Marisa,Binti Yake Mama Taji Mbaraka Mwinshehe Inamaanisha Ni Mjukuu Wa Mwanamuziki Mkongwe Tanzania Hayati Mbaraka Mwishehe.Bado Anasoma Amerecord Hii kwaajili ya Mapenzi Yetu Kwenu..Hiki Ni Kipaji Kitakachochukua Nafasi Kubwa Baadae.

No comments: