22.11.13

Friday, May 31, 2013

(News) TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

 Kama kamati tunaomba kutoa taarifa kwamba mwili wa Ndugu yetu Albert Mangwea utafika siku ya jumapili ya tarehe 2/06/2013 saa nane mchana na sio siku ya jumamosi kama ilivyotaarifiwa hapo awali , Sababu za Mwili wa Albert Mangweha kushindwa kufika jumamosi kama ilivyopangwa ni kutokana Watanzania wenzetu waishio Afrika Kusini kuomba na wao kutoa heshima zao za mwisho . Kwa Maana hiyo basi taratibu zote za kuaga mwili wa Albert Mangweha kwa Wakazi wa Dar es Salaam na maeneo ya Jirani zitafanyika siku ya Jumatatu ya tarehe 03/06/2013 kuanzia saa mbili asubui mpaka saa sita mchana , ambapo baada ya hapo safari rasmi ya kuelekea Morogoro kwa ajili ya mazishi itaanza. Tunaomba radhi kwa usumbufu wote uliojitokeza Asante

No comments: