22.11.13

Wednesday, September 11, 2013

(News) Diamond Platinumz aingia mkataba na Vodacom Tanzania

 Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Kelvin Twissa (katikati) akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa offer ya miito ya simu jijini Dar es Salaam. Kupitio ofa hio, wateja wanaweza kuchukua wimbo wa Diamond Platinumz kama Ring Back Tone (RBT) na wajishindie Tsh50,000 kwa siku. Kushoto ni msanii wa muziki ya kizazi kipya, Diamond Platinumz na kulia ni Meneja wa Mahusiano ya Nje wa Vodacom Tanzania, Salum Mwalim.

 Msanii wa muziki ya kizazi kipya Diamond Platinumz (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa offer ya miito ya simu jijini Dar es Salaam. Kupitia ofa hio, wateja wanaweza kuchukua wimbo wa Diamond Platinumz kama Ring Back Tone (RBT) na wajishindie Tsh50,000 kwa siku. Katikati ni Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Kelvin Twissa (katikati) na kulia ni Salum Mwalim, Mejena wa Mahusiano ya Nje, Vodacom Tanzania.

 Msanii wa muziki ya kizazi kipya Diamond Platinumz (kushoto) akisalimiana na Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Kelvin Twissa, punde baada ya kusaini mkataba utakaowezesha wateja kuchukua wimbo wa Diamond Platinumz kama Ring Back Tone (RBT) na wajishindie Tsh50,000 kwa siku. Anayeshuhudia ni Salum Mwalim , Mejena wa Mahusiano ya Nje, Vodacom Tanzania. 

Msanii wa muziki ya kizazi kipya Diamond Platinumz (mwenye fulana nyekundu) akiucheza wimbo wake mpya ujuikanao kama My Number One, wakati wa uzinduzi wa mkataba utakaowezesha wateja kuchukua wimbo huo kama Ring Back Tone (RBT) na wajishindie Tsh50,000 kwa siku. Mkataba huo ni baina ya Diamond Platinumz na Vodacom Tanzania.

No comments: