22.11.13

Thursday, September 26, 2013

(News) Vodacom yakabidhi vifaa kwa Waziri Mukangala vitakavyotumika kwenye mashindano maalum ya Sekondari

  Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Fenella Mukangala akishirikiana na Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Kelvin Twissa kukagua vifaa vya michezo muda mfupi kabla ya Waziri kukabidhiwa rasmi vifaa hivyo vitakavyotumika kwenye mashindano maalum ya Sekondari Mkoa wa Dar es salaam. Kushoto ni Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim.

  Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Fenella Mukangala akipokea vifaa vya michezo kutoka kwa Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Kelvin Twissa. Vifaa hivyo vitatumika kwenye mashindano maalum ya Sekondari Mkoa wa Dar es salaam. Kushoto ni Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim. Vodacom ilikabidhi jezi za soka seti 12, mipira 40 na kombe kubwa la Mshindi
  Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Fenella Mukangala akipokea kombe kubwa kutoka kwa Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Kelvin Twissa atakalokabidhiwa mshindi wa kwanza wa mashindano maalum kwa shule za sekondari Mkoa wa Dar es salaam yanayoandaliwa na Wizara.Kushoto ni Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim na Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Maendeleo ya Michezo Juliana Yasoda. Vodacom ilikabidhi pia jezi za soka seti 12 na mipira 40.
  Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Fenela Mukangala akiongea na waandishi wa habari wakati wa hafla ya kupokea vifaa mbalimbali vya michezo vilivyotolewa na Vodacom kwa ajili ya mashindano maalum kwa shule za sekondari za mkoa wa Dar es salaam yanayoandaliwa na Wizara.
  Waandishi wa Habari wakimfuatilia Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Fenela Mukangala wakati akiongea kwenye hafla ya kupokea vifaa mbalimbali vya michezo kutoka Vodacom vitakavyotumika kwenye mashindano maalum ya shule za Sekondari Mkoa wa Dar es salaam yanayoandaliwa na Wizara.
  Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Kelvin Twissa akifanunua jambo kwa Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Fenela Mukangala wakati walipofanya mazungumzo mafupi baada ya hafla ya amkabidhiano ya vifaa vya michezo kwa ajili ya mashindano maalum ya shule za Sekondari za Mkoa wa Dar es salaam. Kushoto ni Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim.

No comments: