22.11.13

Tuesday, November 05, 2013

(News) Wafanyakazi Vodacom Tanzania wang’ara Tuzo za mwaka

Dar es Salaam, Novemba 2, 2013 … Wafanyakazi wa kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania wamefanikiwa kunyakua tuzo za utendaji bora za kila Mwaka zinazotolewa na umoja wa makampuni hayo Afrika.
Tuzo hizo ambazo hutolewa kila mwaka kwa watu binafsi na kundi lenye utendaji uliotukuka zimemshuhudia Lilian Mwasha, Mkuu wa Huduma Endelevu, akijinyakulia tuzo ya kujitolea kwa jamii huku Mkuu wa kitengo cha Uendelezaji Biashara, M – pesa,  Isack Nchunda akijishindia tuzo ya utendaji binafsi huku tuzo ya timu bora ikienda kwa kitengo cha mauzo cha kampuni hiyo.
 Akizungumza na wafanyakazi wote wa Vodacom Tanzania nchini, Mkurugenzii Mtendaji wa Kampuni hiyo, Rene Meza amewapongea washindi wa Tuzo hizo kwa utendaji wao uliotukuka katika maeneo yao ya kazi akisema “ Tunajivunia kuwa na aina ya Wafanyakazi wa aina yenu nyie ni nguzo ya kampuni yetu na tunafurahia mafanikio yenu, alisema Meza na Kuongeza,” Tunawatakia mafanikio mema katika utendaji wenu wa kila siku nasi tutaendelea kuwaunga mkono.
Kwa upande wake Ofisa Mkuu Mkuu wa Kitengo cha Rasilimali watu, Fred Mwita, amesema wafanyakazi wa kampuni hiyo wameendelea kujitolea kwa nguvu zao zote na ndio maana Vodacom imeendelea kuongoza katika soko miaka yote.
 “Kila mwaka wafanyakazi wa makampuni ya Vodacom kutoka nchi mbalimbali  ambazo Vodacom inatoa huduma zake ikijumuisha nchi za, Tanzania, Msumbiji, Jamhuri ya Kidemokrasia ya kongo, Afrika ya Kusini na Lesotho, huchaguliwa na kuhudhulia tuzo hizo ambazo hutolewa Johannesburg Afrika ya Kusini.
 “Washindi wa Tuzo hizi huchaguliwa kutokana na utendaji wao wenye tija uliozidi viwango vyao vya majukumu yao ya kila siku, huku tuzo hizo zikiwa sehemu ya kutambua mchango wa wafanyakazi hao na kuwahamasisha wengine.
 “Tunao wafanyakazi ambao wanachaguliwa katika vipengele mbalimbali vya tuzo zinazotolewa na kampuni yetu kuanzia kwa mtu mmoja mmoja na wale wanaojitolea katika kazi na timu bora ambazo zimekuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya kampuni zetu, huku tuzo ya ubunifu ikitolewa kwa kwa mtu ambae amekuwa na ubunifu mzuri katika utendaji wake wa kila siku alisema Meza.
Meza alihitimisha kwa kusema ni jukumu la kila mfanyakazi wa kampuni hiyo kuhakikisha anafanya kazi kwa bidii na kwa moyo wake wote ili kuhakikisa kampuni inafanikiwa na kuendelea kuongeza katika soko na kampuni pia haitoacha kutambua michango ya wafanyakazi wake kama ilivyofanyika sasa.
Mwisho . . .  .

No comments: