Farid Kubanda akiwa nyumbani Mwanza na begani akapewa mkanda kudhihirisha yeye ndio mfalme wa Mwanza kwenye Fiesta One Love.
Mama yangu nimekosea kulitaja jina pale juu, Adam akiwa na B12 wakiwa chini baada ya kuwaita Samaki Samaki wazee wa mduara.
Wasanii wakiwa kwenye basi kama backstage yao maana wakitoka nje tu balaa wananchi wanafurika wakitaka picha
Mwanadafada kutoka Bongo Star Search Baby Madaha ikafika zamu yake na mambo yalikuwa bam bam full mtetemesho.
Ikafikia zamu ya Suma Lee kulitawala jukwaa, hapa akiwa na msanii mwenzake Quick Racka wakiimba wimbo wa Yollanda.
Huyu jamaa bwana, akiwa stejini anakimbiza vibaya sana, sasa ukifikia wimbo wa Pesa hapo ndipo utamjua Madee ndio nani maana anagawa hela kwa mashabiki wake..
Joh Makini aliwakilisha Hip Hop kuanzia muonekano wake mpaka analivyokuwa anaimba jukwaani..ilikuwa safi sana pale alipopanda na mdogo wake Niki wa pili.
Chidi Beeeeeeeeeeenz kama kawa akipanda kwa steji mfuniko unakuwa ule ule haina kuremba, cheki kwanza alivyojipanga kushoto Chiku katikati yeye halafu nyuma Body G.
Baada ya kutoka Mr. Blue akaingia Cowbama vijana kutoka Zizzou Entertainment, Mangwea kama kawaida yake kaingia na kuanza kuwapa freestyle.
Mfalme wa Mwanza Ngosha ze Don akaingia bwana, full kelele alipopanda na Matonya na kuimba Usinikubali Haraka haraka
No comments:
Post a Comment