22.11.13

Friday, February 15, 2013

(Audio) Maua Sama ft.Mwana fa - So Crazy


Jina lake la kisanii ni Maua Sama, Msanii chipukizi kutoka Moshi Tanzania. Akiwa Mwanafunzi wa Mwaka wa Kwanza katika Chuo Cha Ushirika na Biashara Moshi, kwa mara ya kwanza anasikika katika kipindi hiki “Exclusively” katika nyimbo yake ambayo amemshirikisha MwanaFA ikiwa ni nyimbo inayomtambulisha katika ulimwengu wa muziki wa Kizazi Kipya Bongo. Ni Almasi Mchangani ambayo imegunduliwa na MwanaFA baada ya kupata ‘demo’ yake ambayo alifanyia studio za Moshi na kuipeleka mbele ya “Management Team” yake Lifeline/T.I.A ambao moja kwa moja wakamchukua. Maua anafanya kazi chini ya uangalizi wa Lifeline/T.I.A Inc; Label ya Muziki ambayo inasimamia kazi za muziki za MwanaFA, amefanya nyimbo yake “So Crazy” kwa Producer Marco Chali wa MJ Records akimshirikisha MwanaFA. Mipango iliyopo ni kumfanya Maua Sama akawa ni mwimbaji bora wa muziki Tanzania.

9 comments:

Anonymous said...

E bhana choka ee huyu du anaimba noumah yaan,Hili n din mchangan haitaj promo vocal lake linauza sana mzee.Kwa wale wote wanaopenda good music nahic tunaanza kupata kile tunachokitaka

Anonymous said...

ni nomaaaaa..ila hii nyimbo ndo ile ya kwanza aliyofanya na "Throneboy"?

Unknown said...

Anajua

Unknown said...

dah jembe langu la ukweli maua to muccobs keep on hustle ma dia sister ntakusupport forever.oya choka ee right decision kumwona maua kweki anaimba,is hot.kiukweli.jah bles her

goafrandos said...

For the first time tz tumepata mwanadada mwenye vocal za kweli

Anonymous said...

Great stuff!!

Anonymous said...

Huyu mdada ni noumer..wnaojiita ma-star wajipangeee...!

Anonymous said...

Hii ni Version ya pili. ya kwanza alifanya na jamaa anaitwa "Throneboy" jamaa aliua kuliko FA. kiukweli. ukiisearch hiyo track iko huku huku kwa DjChoka. Throneboy kamfunika MwanaFA.

Anonymous said...

dj choka kiukweli uyu dada nimempokea vilivyo na amenibamba ile mbaya na saut yake