22.11.13

Friday, May 31, 2013

(News) RATIBA YA MSIBA WA ALBERT MANGWEHA


Tunapenda kutoa shukurani zetu za dhati kwa watanzania wenzetu kwa ushirikiano wenu katika kipindi hiki kigumu cha msiba wa ndugu yetu Albert Mangweha kilichotokea Afrika Kusini.
-          Katika kufanikisha msiba na mazishi ya ndugu yetu mpendwa tunapenda kuchukua nafasi hii kukaribisha wizara husika, mashirika, makampuni na watu binafsi kutoa michango yenu kupitia mitandao ya simu zifuatazo :
-          Kwa watumiaji wa mtandao Tigo, Nenda kwenye kutoa pesa toa kiasi unachotaka kuchangia  , kisha andika namba ya wakala 00001 ,ambapo litatokea jina la Mangwair Contribution  hapo utakuwa tayari umechangia.

-Tigo: Namna ya kuchangia, Nenda kwenye kutoa pesa , andika namba ya wakala ambayo ni 00001, chagua kiasi unachotaka kuchangia,  Jina litakalokuja ni Mangwair Contribution baada ya hapo utakuwa umechangia.
-          
Mpesa –   0754-967738

Pia kwa kutumia akaunti ya benki ifuatayo:
-          Jina la Akaunti : Kenneth B. Mangweha 
Nambari ya Akaunti: 2012505840 Benki : NMB
Pia kwa niaba ya kamati tunapenda kutoa ratiba kama ifuatavyo:
 Mwili wa Ndugu yetu Albert Mangwea utafika siku ya jumapili ya tarehe 2/06/2013 saa nane mchana na sio siku ya jumamosi kama ilivyotaarifiwa hapo awali ,
Siku Jumatatu  ya tarehe 03/06/2013  kuanzia saa mbili asubui  mpaka saa sita mchana , ambapo baada ya hapo safari rasmi ya  kuelekea Morogoro kwa ajili ya mazishi itaanza.

Tukiamini kila mwenye uwezo atachangia katika kufanikisha shughuli hii tunatanguliza shukurani zetu za dhati. 
Pia tunaomba watanzania mujitokeze kwa wingi katika kuaga mwili wa marehemu katika kuonyesha upendo wetu kwa ndugu yetu Albert Mangweha.

No comments: